Ni Nani Hasa Anayeutawala Ulimwengu?
Swali hilo lenye kuvuta fikira ni kichwa cha trakti ambayo hugawanywa na Mashahidi wa Yehova. Mwaka uliopita mwanamke fulani kutoka Mississippi, Marekani, aliandika hivi: “Wakati mwanamume mmoja mchanga aliponiuliza swali hilo, nilitatizika kuhusu jibu langu.” Yeye akataja hivi: “Ilionekana kwangu kwamba ulimwengu hautawalwi katika njia ambayo Mungu angekubali.”
Halafu yeye akaongeza hivi: “Naona katika Maandiko yaliyotolewa katika trakti hiyo kwamba sikuwa nimeelewa kikamili wakati uliopita kile ambacho Biblia hutuambia juu ya jambo hilo. Moja ya nyimbo zetu za Krismasi, ‘Joy to the World,’ wasema kwamba Mungu anatawala ulimwengu, jambo ambalo, kwa kweli, ni danganyifu.”
Mwanamke huyo alimalizia hivi: “Kwa kawaida huwa siandiki barua aina hii lakini nilihisi mwapaswa kuhakikishiwa kwamba angalau katika kisa hiki, kazi yenu yathaminiwa.”
Mashahidi wa Yehova huwaelekeza watu kwa kile ambacho Biblia husema kuhusu habari muhimu zinazoathiri maisha zetu. Ikiwa ungependa nakala ya trakti iliyotajwa juu au kutamani funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5.