Thamani ya Gazeti Moja la Amkeni!
Katika Agosti 1993, mtu mmoja katika São Paulo, Brazili, alipata nakala ya Amkeni! katika taka. Baada ya kulisoma kwa kupendezwa, alituma barua kwa anwani ya Watch Tower Society katika Brazili. Aliandika hivi: “Tafadhali nitumieni taarifa juu ya funzo la Biblia nyumbani bila malipo. Nina uhakika litanisaidia sana.”
Ombi la huyo mtu lilitumiwa kutaniko moja la Mashahidi wa Yehova karibu na anakoishi. Huyo mtu alitembelewa, na funzo la Biblia likaanzishwa pamoja naye. Katika Septemba 1995, huyo mtu alionyesha wakfu wake kwa Mungu kwa ubatizo wa maji kwenye mkusanyiko mmoja wa Mashahidi.
Thamani ya gazeti moja la Amkeni! haipasi kupuuzwa. Yaliyomo hugusa maisha za watu kwa njia ya kibinafsi. Ikiwa ungependa kupokea jarida hili kwa ukawaida, uliza mmoja wa Mashahidi wa Yehova ama uandike ukitumia anwani ihusuyo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5.