“Aliichapisha Gazetini”
Hilo ndilo msichana mmoja mwenye kuthamini wa Kanada alilosema katika barua ya shukrani kwa Watch Tower Society. Alikuwa ameshiriki katika mashindano ya hotuba ya peupe shuleni, na hotuba yake ilipendeza sana mmoja wa wakaguzi hivi kwamba aliomba hotuba hiyo ipigwe chapa katika gazeti la habari la huko.
Msichana huyo alichaguaje habari yake? “Darasa letu, hasa wasichana, lilikuwa na tatizo la kupiga porojo,” akaeleza. Hivyo akategemeza hotuba yake kwa habari aliyosoma katika Amkeni! Sehemu za hotuba yake yenye kichwa “Porojo Yaweza Kudhuru; Wewe Ungehisije?” zilichapishwa katika The Review, ambalo ni gazeti la habari la huko Niagara Falls, Ontario.
Mwamuzi huyo ambaye alikuwa mmoja wa wakaguzi alivutiwa sana na nini? Ebu ona madondoo fulani kutoka kwenye hotuba ya msichana huyo: “Leo porojo imeenea sana katika jumuiya. Yaweza kusababisha maumivu mengi, kukosa usingizi na hata zaidi hisia zilizoumizwa. . . .
“Haiwezekani kukomesha porojo kwa sababu ni asili ya binadamu kuongea. Jambo ambalo tunaweza kufanya ni kuidhibiti. Mambo machache yanayoweza kutusaidia kwa jambo hili ni: 1. Usiongezee porojo unayosikia. 2. Usisikilize porojo. . . . Kwa kusikiliza porojo, inaweza kuonekana kama unakubaliana na yanayosemwa. 3. Porojo yenye kudhuru yaweza kukufanya uwe mwongo. 4. Shauri bora zaidi ya yote ni kufikiri kabla ya kusema! Jiulize ‘Ningehisije kama jambo hili lingesemwa kunihusu?’”
“Tumia mambo hayo manne,” msichana huyo akamalizia, “na inaelekea utakuwa mtu bora zaidi.”
Hilo ni shauri lenye kutumika kama nini kwa kila mtu, si kwa vijana tu wa shule! Amkeni! hujaribu kutoa habari za kisasa za wakati ufaao juu ya mambo mbalimbali. Ikiwa ungependa kupokea jarida hili kwa ukawaida, mwombe mmoja wa Mashahidi wa Yehova wakati watakapokutembelea, au andika kwa kutumia anwani ihusuyo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5.