Shaka Yake Iliondolewa
Wakati mwanamume mmoja mchanga katika kisiwa cha Karibea cha Jamaika alipokutana na Mashahidi wa Yehova, alikuwa na shaka nyingi kuhusu kuwako kwa Mungu na alikana kupuliziwa kwa Biblia. Hata hivyo, alikubali kwa kusitasita nakala ya kitabu Biblia — Neno la Mungu au la Binadamu? Ziara za kurudia zilifanywa kwake, lakini mwishowe aliwaambia Mashahidi wasirudi tena mpaka atakapowaalika.
“Miezi kadhaa baadaye,” Mashahidi waliripoti, “alipiga simu na kuuliza maswali mengi. Lakini bado alikosoa majibu ya Biblia.”
Baada ya muda fulani, huyo mwanamume mchanga aliangushiwa kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, na funzo la Biblia la kawaida likaanzishwa pamoja naye. Baada ya muda mfupi alieleza: “Sasa naweza kuona kwa nini funzo kama hili ni la lazima.” Alikuwa mwenye shauku nyingi sana juu ya yale aliyokuwa akijifunza hivi kwamba aliomba kujifunza mara mbili kwa juma. Baada ya muda mfupi akaanza kuhudhuria mikutano ya Kikristo kwa ukawaida.
Imani ya mamilioni imeimarishwa kwa kusoma Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? na kwa kujifunza kile kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Ikiwa ungependa kupokea nakala ya vitabu hivi au ungependa mtu fulani aongoze funzo la Biblia nyumbani pamoja nawe, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ihusuyo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5.
[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]
Jalada ya kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?: Funjo la karne ya tatu na hati-kunjo ya Kiebrania ya Esta: The Trustees of the Chester Beatty Library, Dublin; sehemu ya kifua cha Aleksanda Mkubwa: Musei Capitolini, Roma