Tumaini la Msichana Mrusi
Msichana mwenye umri wa miaka 15 katika Ukhta, Urusi, jiji lenye idadi ya watu zaidi ya 100,000 lililo umbali wa kilometa zaidi ya 1,200 kaskazini-mashariki mwa Moscow, alionyesha tamaa ya moyo kwa ajili ya hali bora katika dunia. Alieleza hili katika barua ifuatayo kwa ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova katika Urusi:
“Rafiki yangu aliniambia kwamba kile kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi hufafanua maisha ya Yesu Kristo. Ninapendezwa sana na vitabu vyenu, magazeti, na broshua. Acha nieleze jinsi upendezi huu ulivyositawi. Ulianza kwenye ofisi ya simu wakati nilipoenda kulipia gharama za redio na simu. Hapo nikapata trakti kwenye sakafu. Niliiokota, nikakung’uta mavumbi, na kuanza kusoma hiyo trakti, ambayo ilikuwa na kichwa Kwa Nini Maisha Yamejaa Matatizo Sana?
“Nilisoma juu ya taabu na mateso ambayo watu wanapata, na jalada la trakti lilitolea kielezi ahadi ya maisha mapya katika Paradiso. Ninatumaini kwamba siku fulani itakuja. Kwa kweli nataka kuona watu wote wakiwa wenye furaha, wenye uradhi, na walio na afya na pia niwaone jamaa waliokufa. . . . Ningependa kujua ninalopaswa kufanya ili niwe na tumaini la kuishi katika Paradiso ya kidunia. Ninawaomba mnipelekee habari fulani au vitabu. Ningevilipia na gharama za posta.”
Wewe pia waweza kupokea fasihi ambayo yaweza kukusaidia upate tumaini lililo imara lenye msingi wa Biblia la maisha katika dunia iliyo paradiso. Ikiwa ungependa kupokea nakala ya broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? au ungependa mtu akutembelee nyumbani kwako ili kuongoza funzo la Biblia pamoja nawe bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ihusuyo katika ukurasa wa 5.