Msaada kwa Ndoa Iliyokuwa Inavunjika
Mwanamke kutoka Kisiwa cha Kaskazini ya New Zealand aliandika hivi kuhusu kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia: “Nilipoketi mara ya kwanza kujifunza kichapo hicho, nilihisi kana kwamba ndoa yangu ilikuwa imefikia mahali ambapo ama ‘ningeifanya ifaulu au niivunje.’”
Alieleza malezi yake. “Mama yangu alikuwa amepitia ndoa mbili zilizokuwa mbaya sana. Likiwa tokeo, sikuzote tulifunzwa kuwa wanaume walikuwa hawafai kitu na kwamba nia yao ilikuwa kuwaonea wanawake. Kwa hiyo nilikua nikiwa mkaidi sana, mwanamke mwenye kichwa kigumu ambaye hangeghairi kutoka kwa bishano.”
Mwanamke huyo alitambua uhitaji wa mabadiliko. “Niling’amua kwamba kwa sababu ya kutojitiisha kwa mume wangu na kwa sababu nilikuwa mwenye kiburi sana, nilikuwa nikikatisha uwezekano wa furaha ya familia.” Kwa hiyo alifanya marekebisho muhimu, kama anavyoeleza: “Sasa mume wangu nami twajifunza kitabu hicho tukiwa familia, na bado ninaendelea kujifunza jinsi ya kuwa mke Mkristo. Tunafurahia sana uhusiano wetu wa sasa lakini tuna mengi sana ya kufanyia maendeleo.
“Nyumba yetu haijawa kamwe na upendo na utulivu kama ilivyo leo.”
Ikiwa ungependa kupokea nakala ya broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? yenye kurasa 32, ambamo Somo la 8 lazungumzia “Maisha ya Familia Yanayompendeza Mungu,” andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au kwa anwani ihusuyo iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5. Ikiwa ungependa pia mtu fulani aongoze nawe funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali taja jambo hilo.
[Picha katika ukurasa wa 32]
Mungu Anataka Tufanye Nini?