Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g98 8/22 uku. 32
  • ‘Linaburudisha Katika Ulimwengu Huu Wenye Msukosuko’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Linaburudisha Katika Ulimwengu Huu Wenye Msukosuko’
  • Amkeni!—1998
Amkeni!—1998
g98 8/22 uku. 32

‘Linaburudisha Katika Ulimwengu Huu Wenye Msukosuko’

NDIVYO Igor mwenye umri wa miaka 22 kutoka Yugoslavia alivyolifafanua gazeti Mnara wa Mlinzi katika barua mwaka jana. Alieleza hivi:

“Nilianza kusoma gazeti Mnara wa Mlinzi miezi kadhaa iliyopita. Ninasoma matoleo mapya na ya zamani ya Mnara wa Mlinzi (kutoka 1991), na nayapenda sana. Nafikiri gazeti kama hili linaburudisha kwelikweli katika ulimwengu huu wenye msukosuko.

“Makala mlizochapisha kuhusu wamishonari zilinipendeza hasa, na ndiyo sababu nawaandikia. Kwanza, nataka kujua kama naweza kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Mimi ni Mkatoliki, lakini nafikiri kwamba dini yenu ni bora zaidi kuliko nyingine yoyote, hasa kwa sababu hakuna dini nyingine inayojitahidi sana kueneza Neno la Mungu.

“Ikiwa kuwa Mkatoliki si kizuizi, nataka kujua jinsi ninavyoweza kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Nina tamaa moja tu. Ikiwa itawezekana ningependa kubatizwa katika Belgrade. Ikiwa jambo hili litawezekana, tafadhali nijulisheni wakati ninaopaswa kuja na ikiwa kuna sharti lolote kwa ubatizo. Ikiwa haiwezekani, tafadhali niarifuni ni lini ninapoweza kubatizwa na ni nani ninayepaswa kumfikia kwa ajili ya jambo hili.

“Kisha ningetaka kujua jinsi mtu anavyoweza kuwa mishonari. Ningependa kujua ikiwa naweza kuanza kujizoeza kwa ajili ya utumishi wa mishonari mara tu baada ya kubatizwa. Je, ni lazima mtu awe ametumika kwa miaka kadhaa akiwa Shahidi? . . .

“Tafadhali ifikirieni barua yangu kwa uzito. Ninafikiri kwamba kuwa mishonari ndiyo njia bora zaidi ya kueneza habari njema za Ufalme wa Mungu”

Katika ukurasa wa 2 wa kila toleo la Mnara wa Mlinzi kusudi la gazeti hilo linaelezwa hivi: “Hufariji jamii zote za watu kwa habari njema za kwamba karibuni Ufalme wa Mungu utaharibu wale wanaoonea wanadamu wenzao na kwamba utaigeuza dunia iwe paradiso.” Ikiwa ungependa nakala au ungependa mtu akutembelee nyumbani kwako ili kuongoza funzo la Biblia pamoja nawe bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ihusuyo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki