Ni Wapi Tuwezapo Kupata Majibu?
Watu wengi zaidi na zaidi wanazidiwa na matatizo na maswali magumu yanayowakabili leo. Tuoneje kusema uwongo? Je, inafaa kucheza kamari? Namna gani kujihusisha na uwasiliani-roho? Tuoneje utoaji-mimba? Je, ni vibaya kulewa au kwa watu wawili wasiofunga ndoa kufanya ngono?
Maswali ni mengi. Na yanaathiri si maisha zetu tu bali na za wapendwa wetu pia. Watu wanataka majibu yatakayowanufaisha. Mtu mmoja wa aina hiyo, kutoka Mississippi, Marekani, aliandikia Watch Tower Society kama ifuatavyo:
“Katika jalada la nyuma la kitabu chenu Siri ya Kupata Furaha ya Familia, niliona swali lililochapishwa linalouliza ikiwa ningependa habari zaidi au funzo la Biblia la nyumbani bila malipo. Kwa kweli, ningependa!
“Tangu kiangazi cha mwaka wa 1995, nimekuwa nikisoma na kujifunza Biblia. Najaribu kadiri niwezavyo kuielewa Biblia ili kuitumia kwa makusudi yangu ya kiroho na, lililo la maana hata zaidi, kwa kuwafundisha wengine. Ikiwa mwasema mnapeleka habari bila malipo, bila shaka ningependa kuipokea!”
Ikiwa wewe pia ungependa kupokea nakala ya kitabu chenye kurasa 192 Siri ya Kupata Furaha ya Familia au ungependa mtu fulani ajifunze nawe Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ihusuyo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5.