Ina Uvutano Mkubwa
“BROSHUA mnayochapisha Mungu Anataka Tufanye Nini? ilikuwa nzuri sana. Mimi nina umri wa miaka kumi tu, lakini naielewa, nayo ilikuwa rahisi kusoma. Niliielewa vizuri sana, na nilipofika somo la 16, sikutaka kulisoma kwanza kwa sababu niliipenda broshua hiyo sana. Nilitaka kuwe na mengi zaidi.”
Broshua hiyo, jalada unaloona hapa, haikuchapishwa kwa ajili ya watoto pekee. Lakini habari hiyo imetokezwa kwa njia iliyo wazi, sahili hivi kwamba watoto wanaweza kuelewa mafundisho ya msingi ya Biblia na aina ya mwenendo ambao Mungu anataka kutoka kwetu. Kwa kielelezo, broshua hiyo yajibu maswali kama vile: Tuoneje kusema uwongo? Je, inafaa kucheza kamari? Je, ni vibaya kulewa? Je, yafaa watu wasiooana kufanya ngono?
Ukiandikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au kwa kutumia anwani ifaayo kwenye ukurasa wa 5, tutafurahi kukupelekea bila malipo broshua hii yenye kurasa 32 Mungu Anataka Tufanye Nini? Masomo yake 16 yamekusudiwa kuwa mtaala wa funzo la Biblia. Baadhi ya masomo hayo yana kichwa “Ni Nini Kusudi la Mungu kwa Dunia?,” “Ufalme wa Mungu Ni Nini?,” “Maisha ya Familia Yanayompendeza Mungu,” na “Mazoea Ambayo Mungu Huchukia.”
□ Nipelekeeni broshua Mungu Anataka Tufanye Nini?
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.