Asaidiwa Kupata Majibu
MAISHA ni magumu kwa watu wengi ulimwenguni pote, na wengine wanatafuta sababu kwa nini hali iko hivyo. Mwanamume mmoja mwenye umri wa miaka 35 ambaye ana watoto wawili aliandika hivi kutoka jiji la Grodno, Belarus:
“Mwanamke fulani alinisimamisha barabarani akanitolea gazeti la Amkeni! Kwa sababu gazeti hilo lilikuwa lenye kupendeza kwa nje, nililichukua ingawa sikujua linazungumzia nini. Nilipofika nyumbani, nilitazama makala zake, zikanipendeza.
“Sijioni kuwa mwamini. Hata hivyo, katika kichapo chenu nilipata majibu yenye kutegemeka kwa maswali mengi yaliyokuwa yakinisumbua. Maisha yetu si rahisi sasa, na tunahitaji hasa msaada wa Biblia. Nawaomba mniletee habari zaidi juu ya Mungu na mafundisho yake. Kwa muda mrefu nimetafuta majibu kwa maswali mengi, na kichapo chenu kimenisaidia kupata majibu.”
Kichapo kimoja chenye thamani ambacho kimesaidia mamilioni ya watu ni ile broshua yenye kurasa 32 Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje? Waweza kupokea nakala kwa kujaza na kupeleka kuponi iliyopo hapa ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani inayohusu iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili. Onyesha lugha ipi
□ Nipelekeeni nakala ya broshua Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje?
◻ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.