Unaalikwa kwa Moyo Mkunjufu
KIFO cha mwanamume Yesu Kristo zaidi ya miaka 1,900 iliyopita kilikuwa tukio la maana zaidi katika historia. Kilifungua njia ya matazamio ya kupata uhai udumuo milele chini ya hali za Paradiso. Wakati wa mwadhimisho sahili, Yesu alitumia divai na mkate usiotiwa chachu vikiwa mifano ya dhabihu yenye upendo ya kibinadamu. Kisha akawaambia wanafunzi wake hivi: “Fulizeni kufanya hili katika ukumbuko wangu.” (Luka 22:19) Je, utakumbuka?
Mashahidi wa Yehova wanakualika kwa uchangamfu ujiunge nao kuadhimisha sherehe hii ya Ukumbusho. Itafanywa baada ya jua kushuka tarehe inayolingana na Nisani 14 kwenye kalenda ya mwezi ya Biblia. Unaweza kuhudhuria kwenye Jumba la Ufalme lililo karibu na nyumbani kwako. Uliza Mashahidi wa Yehova wa kwenu saa na mahali hasa. Tarehe ya sherehe hiyo mwaka huu ni Alhamisi, Aprili 1.