Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g01 11/8 uku. 32
  • Watoto Wapaswa Kutiwa Nidhamu Vipi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watoto Wapaswa Kutiwa Nidhamu Vipi?
  • Amkeni!—2001
Amkeni!—2001
g01 11/8 uku. 32

Watoto Wapaswa Kutiwa Nidhamu Vipi?

Gazeti la National Post la Kanada lilisema hivi: “Matatizo hutokea watoto wanapoambiwa kwamba wao ni wazuri haidhuru wanachofanya.” Wazazi fulani huamini kwamba kufanya hivyo huwawezesha watoto wao kujiheshimu. Hata hivyo, kulingana na mwanasaikolojia Roy Baumeister, ‘si vibaya kujiheshimu kwa sababu ya kutimiza jambo zuri, lakini wazazi wapaswa kuwafunza watoto hasa kujidhibiti.’

Mzazi anayeogopa kumrekebisha mtoto wake wakati anapokosea anamwumiza kijana huyo. Kwani, kutia nidhamu ni mbinu ya kufundisha. Hivyo, nidhamu humfunza mtoto aliyekosea asirudie makosa. Bila shaka, wazazi wapaswa kuepuka kutoa nidhamu kwa njia ya ukali au inayozidi makosa yaliyofanywa. (Yeremia 46:28) Wanapaswa kuhakikisha kwamba nidhamu haipiti kiasi. Biblia husema hivi: “Nyinyi akina baba, msiwe mkichochea watoto wenu wakasirike, ili wasishuke moyo.”—Wakolosai 3:21.

Kwa kawaida, Biblia huhusianisha nidhamu pamoja na upendo na upole, wala si pamoja na hasira na ukatili. Mshauri stadi apaswa kuwa ‘mwanana kuelekea wote, . . . akijizuia mwenyewe chini ya uovu, akiagiza kwa upole wale wasio na mwelekeo ufaao.’ (2 Timotheo 2:24, 25) Kwa hiyo, mzazi hapaswi kutoa nidhamu ili kuondoa hasira tu. Biblia haimruhusu kutumia njia zinazoweza kumuumiza mtoto.

Mamilioni ya watu ulimwenguni kote wamenufaishwa na kichapo cha kurasa 192 chenye kichwa Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Miongoni mwa sura zake zenye kuelimisha ni “Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana” na “Saidia Tineja Wako Asitawi.” Ili upate nakala yako, tafadhali jaza kuponi iliyo hapa na uitume kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili. Utapata madokezo hususa yanayoweza kukusaidia kutatua matatizo na kufanya maisha ya familia yafurahishe kama Muumba alivyokusudia.

□ Nitumieni nakala ya kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Onyesha lugha unayotaka.

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki