“Ni Nyinyi Pekee Mnaoweza Kunisadia
NDIVYO DAKTARI MMOJA kwenye Chuo Kikuu cha Tiba cha Kaunas huko Lithuania alivyomalizia barua aliyotuma kwenye ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova nchini humo. Daktari huyo alisema hivi:
“Nilianza kusoma kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi nilipokuwa kazini. Nilinuia kutumia habari kutoka kwa kitabu hicho katika makala kadhaa nilizopanga kuandika, lakini kitabu hicho kikapotea. Yaelekea mtu fulani alikichukua. Niliudhika kwa sababu nilipoteza kitu cha maana sana. Tafadhali nitumieni nakala nyingine.
“Ninahitaji kitabu hicho sana kwa kuwa mimi hutembelea shule mbalimbali na kutumia wakati pamoja na vijana, na kitabu hicho hunisaidia kujibu maswali yao mengi. Nikipata nakala nyingine, nitaiweka nyumbani na kuitunza vizuri. Kitabu hicho ni muhimu sana na ndiyo sababu mtu fulani alikichukua. Katika siku hizi zenye taabu, tunahitaji kutiwa moyo. Ni nyinyi pekee mnaoweza kunisaidia.”
Kitabu Vijana Huuliza kinajibu maswali mengi ambayo vijana hujiuliza, kama vile: “Niwafanyeje Wazazi Wangu Wanipe Uhuru Zaidi?,” “Je! Niondoke Nyumbani?,” “Naweza Kufanyaje Marafiki wa Kweli?,” “Nichague Kazi-Maisha Gani?,” “Vipi Juu ya Ngono Kabla ya Ndoa?,” na “Nijueje Kama Ni Upendo Halisi?” Hizo ni sura chache tu katika kitabu hicho. Unaweza kuomba nakala ya kitabu hicho kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma kwenye anwani iliyoonyeshwa au kwenye anwani inayofaa iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nitumieni kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi.
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.