‘Wanafunzi Hulisoma kwa Ukawaida’
MFANYAKAZI mmoja wa maktaba huko Divinópolis, katika jimbo la Minas Gerais nchini Brazili, aliandikia ofisi ya Mashahidi wa Yehova nchini humo akieleza jinsi wanafunzi wanavyopendezwa sana na gazeti la Amkeni! Alieleza hivi:
“Katika maktaba ya shule ya manispaa ninakofanya kazi, nyakati nyingine sisi hupokea misaada ya vitabu vilivyochapishwa na [Mashahidi wa Yehova]. Ingawa hakuna hata mmoja ambaye ni Shahidi wa Yehova, wanafunzi hulisoma Amkeni! kwa ukawaida wakifanya utafiti kuhusu mambo mbalimbali. Kwa mfano, toleo la Septemba 8, 2000, limekuwa muhimu sana kwa sababu lina habari nzuri kuhusu Michezo ya Olimpiki. Kwa sababu hiyo, ningependa kuwaomba mtupatie matoleo mengi tofauti-tofauti ya Amkeni! Nina hakika kwamba mnapendezwa kama mimi kuwapa wachanga wetu habari za kusoma zenye kujenga.”
Katika ukurasa wa 4, kila toleo la Amkeni! hueleza ni kwa nini gazeti hili huchapishwa. “La maana kuliko yote,” hilo hueleza, “gazeti hili hujenga uhakika katika ahadi ya Muumba ya kuleta ulimwengu mpya wenye amani na usalama ambao uko karibu kuchukua mahali pa mfumo wa mambo uliopo mwovu na usiotii sheria.”
Mashahidi wa Yehova pia hutoa broshua ambazo zimetayarishwa kutimiza kusudi hilo, mojawapo ya broshua hizo inaitwa Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai? Wewe Waweza Kulipataje? Unaweza kuomba nakala moja kwa kujaza na kutuma kuponi iliyo hapa kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 4 wa gazeti hili.
□ Nitumie broshua Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai? Wewe Waweza Kulipataje?
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.