Unaalikwa Je, Utakuwepo?
UNAALIKWA WAPI? Kwenye mkutano muhimu zaidi unaofanywa kila mwaka na Mashahidi wa Yehova wa kukumbuka kifo cha Kristo, unaotegemea Mlo wa Jioni wa Bwana ambao Kristo alianzisha. Simulizi la Mathayo latueleza hivi: “Yesu alichukua mkate na, baada ya kusema baraka, akaumega na, akiwapa wanafunzi, akasema: ‘Chukueni, kuleni. Huu wamaanisha mwili wangu.’ Pia, alichukua kikombe na, akiisha kushukuru, akawapa hicho, akisema: ‘Nyweni kutoka hicho, nyinyi nyote; kwa maana hii yamaanisha “damu yangu ya agano,” inayopaswa kumwagwa kwa niaba ya wengi kwa msamaha wa dhambi.’”—Mathayo 26:26-28.
Umuhimu wa maneno hayo utaelezwa kwenye sherehe ya mwaka huu ya Mlo wa Jioni wa Bwana, mnamo Alhamisi, Machi 28, baada ya jua kushuka. Twatumaini kwamba utakuwepo. Tafadhali waulize Mashahidi wa Yehova juu ya saa kamili na mahala pa kukutana katika eneo lako. Unakaribishwa sana.