Alilipata Katika Duka Linalonunua Karatasi Kuukuu
KIJANA mmoja anayesema Kitamil huko Chennai, India, aliliona toleo la gazeti la Amkeni! la Agosti 8, 1999 katika duka linalonunua karatasi kuukuu. Baada ya kusoma gazeti hilo, na matoleo mengine aliyoweza kupata, aliandika maoni yake na kuyatuma kwenye ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova huko India.
Aliandika hivi: “Amkeni! ni gazeti bora, lenye kuelimisha na lenye manufaa. Habari zinazozungumziwa ni zenye faida. Hongera!”
Kisha kijana huyo aliomba hivi: “Ningependa sana kuwa na gazeti hilo lenye kuelimisha katika maktaba yangu, kwa kuwa linazungumzia habari za kila sehemu ya dunia. Baada ya kusoma matoleo yaliyochapishwa hadi leo, ningependa sana kupata matoleo yatakayofuata.”
Kama inavyoelezwa kwenye ukurasa wa 4 wa kila gazeti, Amkeni! huelimisha watu kuhusu mambo mbalimbali. Hata hivyo, kusudi maalumu la gazeti hili husema hivi: “La maana kuliko yote, gazeti hili hujenga uhakika katika ahadi ya Muumba ya kuleta ulimwengu mpya wenye amani na usalama ambao uko karibu kuchukua mahali pa mfumo wa mambo uliopo mwovu na usiotii sheria.”
Kichapo chenye kurasa 32 cha Mungu Anataka Tufanye Nini? chakazia kusudi hilo la Mungu na kuonyesha kile ambacho Biblia inasema tunahitaji kufanya ili kupata kibali chake. Unaweza kuomba nakala ya kichapo hicho kwa kujaza kuponi iliyopo hapa chini na kuituma kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nitumieni kichapo Mungu Anataka Tufanye Nini?
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.