Kitabu Kinachoweza Kusaidia Kuokoa Ndoa
MWAKA ULIOPITA, mwanamke anayeitwa Leslie, anayeishi huko Louisiana, Marekani, alipigiwa simu na mwakilishi wa Chuo Kikuu cha Tulane. Mwakilishi huyo alisema kwamba chuo hicho, na chuo kingine pia, kilikuwa kikifanya uchunguzi kuhusu wale waliofunga ndoa hivi majuzi huko Louisiana.
Mwanamke huyo alikubali kushiriki katika uchunguzi huo, naye akatumiwa barua yenye orodha ya maswali. Alijibu maswali hayo na akarudisha karatasi hiyo pamoja na kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Alieleza kwamba yeye na mumewe ni Mashahidi wa Yehova na kwamba walijifunza kitabu hicho pamoja kabla ya kufunga ndoa.
Majuma machache baadaye, msimamizi wa mradi huo alimtumia barua iliyosema hivi: “Tuna hakika kwamba wenzi wa ndoa kama wewe na mumeo wanaweza kutufundisha jinsi ya kufanya ndoa iwe imara na yenye furaha. Mlilelewa katika mazingira tofauti na mara nyingi jambo hilo laweza kusababisha hali ya kutoelewana katika ndoa. Lakini kwa kuwa mlijitayarisha kwa ajili ya ndoa, hasa kwa kutumia vitabu kama kile ambacho mlituma, mtaweza kushughulikia magumu yoyote ambayo huenda yakatokea. Na bila shaka, dini ni muhimu sana katika ndoa. Ni vizuri kwamba nyote mna imani moja thabiti na mnategemea msaada wa Mungu.
“Nimeweka kitabu ulichotuma kwenye dawati langu, nami huwaonyesha wanafunzi wangu kitabu hicho wanapoomba ushauri kuhusu ndoa. Sikuwa nimeona kitabu hicho hapo awali. Ni kizuri sana.”
Twatumai kwamba kitabu hicho kitakusaidia sana. Ili upate nakala yako, tafadhali jaza kuponi iliyo hapa chini na uitume kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili. Utapata madokezo hususa yanayoweza kukusaidia kutatua matatizo na kufanya maisha ya familia yafurahishe kama vile Muumba alivyokusudia.
□ Nitumieni nakala ya kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia.
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.