“Kitabu Kidogo Chenye Ujumbe Wenye Nguvu”
Kijana mmoja alipoacha kazi yake ya benki huko Chicago, Illinois, Marekani, ili kuongeza elimu yake, mfanyakazi mwenzake alimpatia kitabu Je Kuna Muumba Anayekujali? Baadaye alipokea barua kutoka kwa mwanamume huyo, aliyeandika hivi:
‘Ulinipatia kitabu kidogo chenye ujumbe wenye nguvu sana! Nimekuwa nikikisoma kwa majuma machache yaliyopita, na kimeeleza mambo kwa ufahamu wenye kina. Hasa nilipendezwa na jinsi uthibitisho wa sayansi ya anga na jiolojia umetumiwa kuonyesha kwamba uumbaji ni “tendo lililopangwa na mtu mwenye akili.” Pia nilifurahia jinsi ambavyo kimekazia sana Mahubiri ya Mlimani.’
Baada ya kusoma kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? wengi wamechochewa kufikiri kwa uzito zaidi kuhusu chanzo cha uhai na kusudi lake. Jambo la maana hata zaidi ni kwamba wengi wamesaidiwa kufikia uamuzi wenye hekima.
Unaweza kuomba kitabu hicho chenye kurasa 192 kwa kujaza kuponi iliyo hapa chini na kuituma kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nitumieni kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali?
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.
[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]
Juu: Courtesy of Anglo-Australian Observatory, photograph by David Malin; jalada: J. Hester and P. Scowen (AZ State Univ.), NASA