“Nilivutiwa na Upendo Alioonyesha”
Mwanamume mmoja katika jiji la Nis aliandika hivi katika barua aliyotuma kwenye ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova nchini Yugoslavia:
“Kila siku mimi husoma sura kadhaa katika Biblia, na ninafurahia sana kufanya hivyo. Siku hizi ninasoma pia kichapo Mungu Anataka Tufanye Nini? Ninataka kuwashukuru kwa kichapo hicho kizuri kinachoeleza Biblia. Mambo yote katika kijitabu hicho yameelezwa kwa njia rahisi na yenye kueleweka.
“Ninapendezwa hasa na somo linalomhusu Yesu Kristo. Nilivutiwa na upendo alioonyesha alipotoa uhai wake mkamilifu kwa ajili ya watu ambao hata hakuwajua. Kila mtu anapaswa kutambua dhabihu yake na kuithamini.”
Tuna hakika kwamba hata wewe utafaidika kusoma kichapo hicho chenye kurasa 32, Mungu Anataka Tufanye Nini? Mbali na somo lake lenye kupendeza “Yesu Kristo Ni Nani?,” kuna masomo mengine kama vile “Mungu Ni Nani?,” “Ni Nini Kusudi la Mungu kwa Dunia?,” na “Ufalme wa Mungu Ni Nini?” Unaweza kuomba nakala yako kwa kujaza kuponi iliyo hapa chini na kuituma kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nitumieni kichapo Mungu Anataka Tufanye Nini?
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.