“Ilikuja kwa Wakati Unaofaa”
HIVYO ndivyo alivyoandika mwanamume mmoja kutoka jiji la Abakaliki katika barua aliyoituma kwa ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova huko Nigeria. Alikuwa akizungumza kuhusu broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, ambayo alikuwa amepewa majuzi. Yeye alieleza hivi:
“Mke wangu mpendwa, Tochi, alikufa muda mfupi baada ya kujifungua mnamo Juni 18, 2000. Kwa zaidi ya mwezi mmoja baada ya tukio hilo, nilikumbwa na mshtuko, kutokuwa na hisia, utupu, na hali ya kutokuamini msiba huo mbaya sana uliowahi kunipata. Kisha katika mwezi wa Julai, mmoja wa Mashahidi wa Yehova alinipatia nakala ya kichapo chenu kinachoitwa Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. Broshua hiyo ilikuwa kwangu kama dawa, na sasa ninaendelea kupata nafuu polepole kupitia msaada wa mashauri ambayo broshua hiyo imetoa. Broshua hiyo ilinipa tumaini jipya na kunifanya nione kwamba kuna sababu ya kutazamia mema katika hali yangu yenye kuvunja moyo sana.”
Huenda hata wewe au mtu unayemjua akafarijiwa kwa kusoma broshua hiyo yenye kurasa 32. Unaweza kuomba nakala moja kwa kujaza kuponi iliyo hapa chini na kuituma kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nitumieni broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. Onyesha lugha unayotaka.
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.