Kupata Hazina Katika Chumba cha Kanisa Kilichoko Chini ya Ardhi
Mwaka uliopita mwanamke mmoja katika jimbo la New York, Marekani, aliripoti jinsi alivyopata hazina. Katika barua yake iliyoelekezwa kwa “Yeyote Anayehusika,” yeye aliandika hivi: “Nilikipata kitabu hicho kidogo katika chumba cha kanisa la kwetu kilichoko chini ya ardhi, kisha nikakipeleka nyumbani. Kitabu hicho kina kichwa Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani.”
Mwanamke huyo alieleza hivi: “Sasa, nimebakiza sura nne tu nimalize kukisoma kwa mara ya pili. Kilinipendeza sana hivi kwamba ilinibidi kukisoma kwa mara ya pili, polepole, ili nielewe kila jambo waziwazi. Nimejifunza mambo mengi zaidi kutokana nacho kuliko yale ambayo nimejifunza katika kanisa langu. Na nimejifunza mambo ambayo sikuwahi kuyajua kamwe. Ninatamani kuwa na vitabu vingine vidogo kama hicho.”
Kitabu hicho kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova miaka 20 iliyopita, na zaidi ya nakala milioni 81 zilichapwa katika lugha 112. Ingawa hakichapwi sasa, unaweza kusoma mambo yake makuu katika broshua za kurasa 32 zinazoitwa Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai? Wewe Waweza Kulipataje? na Je! Kweli Mungu Anatujali?
Unaweza kuomba nakala mojamoja ya broshua hizo mbili kwa kujaza kuponi iliyo hapa chini na kuituma kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nitumieni nakala ya broshua Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai? Wewe Waweza Kulipataje? na Je! Kweli Mungu Anatujali?
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.