Wote Walikikubali
Katika shule moja huko Basel, Uswisi, mwalimu aliwaambia wanafunzi watayarishe hotuba ya dakika 10 hadi 15 kuhusu habari yoyote ile. Rosi, mwenye umri wa miaka 15 alichagua kichwa “Kupata Faida Zote za Ujana Wako.”
Wanafunzi wenzake walimuuliza hivi: “Hicho ni kichwa cha aina gani? Je, utazungumza kuhusu dawa za kulevya?”
Akajibu, “subirini, mtaona.”
Alipomaliza hotuba yake, wanafunzi walipiga makofi. Kisha Rosi akasema: “Kwa kweli, dakika 15 hazitoshi kueleza jinsi ya kupata faida zote za ujana wako.” Halafu akasema: “Nitawapa ninyi nyote zawadi.” Akampa kila mwanafunzi kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi. Kwa ujumla aliwapa vitabu 20 vilivyokuwa vimefunikwa vizuri na kuandikwa jina la kila mwanafunzi.
Wanafunzi wote walikubali kitabu hicho kwa furaha na baadaye walionekana wakichunguza sura zilizomo, kutia ndani sura zifuatazo: “Niwafanyeje Wazazi Wangu Wanipe Uhuru Zaidi?,” “Naweza Kufanyaje Marafiki wa Kweli?,” “Nichague Kazi-Maisha Gani?,” “Vipi Juu ya Ngono Kabla ya Ndoa?,” na “Nijueje Kama Ni Upendo Halisi?”
Kitabu hicho kina jumla ya sura 39. Unaweza kuomba nakala ya kitabu hicho kwa kujaza na kutuma kuponi iliyo hapa kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nitumieni nakala ya kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi.
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.