“Nilitaka Kujua Zaidi”
MWAKA uliopita mwanamke mmoja aliandika hivi: “Jana nilipokea kichapo Mungu Anataka Tufanye Nini? nilichoagiza kupitia barua.” Alieleza kwamba kabla ya hapo alikuwa ameona matangazo mawili kuhusu kichapo hicho. “Nilikingojea kwa hamu kwa sababu niliposoma matangazo hayo nilitaka kujua zaidi,” alisema. Nilipopokea kichapo hicho, nilianza kukisoma mara moja. Mambo yote niliyosoma katika kichapo chenu ni ya kweli na yanatokana na Biblia.”
Alimalizia hivi: “Ninahisi uharaka wa kutenda kulingana na mambo niliyosoma.”
Tunaamini wewe pia utafaidika kwa kusoma kichapo hicho chenye kurasa 32 Mungu Anataka Tufanye Nini? Zaidi ya kuwa na somo la kupendeza kuhusu “Yesu Kristo Ni Nani?” utapata masomo mengine, kama “Mungu Ni Nani?,” “Ni Nini Kusudi la Mungu kwa Dunia?,” na “Ufalme wa Mungu Ni Nini?” Ukitaka kuomba nakala moja, jaza nafasi iliyo hapa chini na kuituma kwenye anwani iliyoonyeshwa au anwani inayofaa iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nitumieni broshua Mungu Anataka Tufanye Nini?
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.