‘Nilimpata Tena Yesu Aliyekuwa Amesahauliwa’
Aliposoma kitabu “Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi,” mwanamke mmoja kutoka Saint-Jérôme, Quebec, Kanada, aliandika hivi: “Nilifurahi sana kwa kumpata tena Yesu aliyekuwa amesahauliwa, ambaye mara nyingi huchorwa kwa njia isiyo sahihi.”
Mwanamke huyo alisema hivi kuhusu michoro iliyo katika kitabu hicho: “Nilivutiwa sana na michoro iliyo katika kitabu chenu. Kwa maoni yangu watu ambao wamechorwa katika kitabu hicho wanaonekana kama watu halisi walioishi siku za Yesu alipokuwa akihubiri.” Alimalizia kusema: “Nawapongeza kwa kutayarisha kitabu hicho. Kitabu hicho kinatoa mwelekezo bora wa kuwasaidia watu wanaotaka kujifunza zaidi kuhusu mafundisho ya kweli ya Yesu.”
Kitabu Mtu Mkuu hujaribu kueleza kila tukio katika maisha ya Yesu alipokuwa duniani kulingana na masimulizi ya vitabu vinne vya Injili, kutia ndani hotuba alizotoa na mifano na miujiza yake. Kwa kadiri inavyowezekana, kila jambo limeelezwa kwa kufuata wakati unaodhaniwa kuwa lilitokea. Na kama ilivyoonyeshwa tayari, kitabu hicho kina michoro maridadi, inayoonyesha matukio halisi ambayo imekusudiwa kuonyesha hisia za Yesu na za wale walioishi wakati wake.
Iwapo ungependa kupokea kitabu hicho chenye kurasa 448, tafadhali jaza na utume kuponi iliyo hapa chini kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nitumieni kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi.
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.