Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g03 2/22 uku. 32
  • “Wakati Huu Ilinigusa Moyo”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Wakati Huu Ilinigusa Moyo”
  • Amkeni!—2003
Amkeni!—2003
g03 2/22 uku. 32

“Wakati Huu Ilinigusa Moyo”

Mnamo mwaka wa 1994, Mashahidi wa Yehova walichapisha broshua inayozungumzia ugumu wa kukabiliana na kifo cha mpendwa. Broshua hiyo imewafariji watu wengi.

Hivi majuzi, msomaji mmoja mwenye shukrani kutoka Pennsylvania, Marekani, aliandika hivi: “Nilipoipokea broshua hiyo mara ya kwanza, niliwaza ‘Ni nzuri sana.’ Hata hivyo, sikutambua thamani yake hadi nilipompoteza binti yangu majuma mawili yaliyopita. Nilihuzunika sana na nikaanza kuisoma ili nipate msaada. Wakati huu ilinigusa moyo. Inataja mambo yote yaliyoniumiza, na ilinifariji.”

Broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa hujibu maswali kama: Ninawezaje kuishi na huzuni yangu? Wengine waweza kusaidiaje? Kuna tumaini gani kwa wafu?

Huenda wewe au mtu mwingine unayemjua akapata faraja kwa kusoma broshua hiyo yenye kurasa 32. Unaweza kuomba broshua hiyo kwa kujaza na kutuma kuponi iliyo hapa kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani inayofaa iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Nitumieni broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. Onyesha lugha unayotaka.

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki