Tukio Muhimu Zaidi Katika Historia
Tukio hilo lilikuwa kifo cha Yesu Kristo. Kwa nini lilikuwa muhimu?
Ni kwa sababu lilisaidia kutetea uadilifu wa Mungu, na kuthibitisha kwamba wanadamu wanaweza kudumisha utimilifu kikamilifu kwa Mungu.
Tukio hilo liliwapa wanadamu taraja la kupata uzima wa milele katika dunia Paradiso.
Yesu mwenyewe alianzisha ukumbusho wa kifo chake usiku ulitangulia kifo chake. Ilikuwa sherehe isiyohusisha mambo mengi. Wakati huo, Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”—Luka 22:19, 20.
Je, utalikumbuka?
Mashahidi wa Yehova wanakukaribisha ujiunge nao katika kukumbuka tukio hilo muhimu zaidi katika historia. Mwaka huu Ukumbusho huo utafanywa Jumamosi, Machi 22, baada ya jua kushuka. Tafadhali waulize Mashahidi wa kwenu saa za kuanza na mahali pa kufanywa. Hakuna sadaka zitakazokusanywa, na wageni wanakaribishwa wasikilize hotuba yenye kujenga na kuona sherehe hiyo isiyohusisha mambo mengi.