Kinawasaidia Kuwa na Maisha Yenye Kusudi
◼ Kitabu ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’ kimekuwa na matokeo mazuri kwa watu wengi wanaokisoma. “Kimenisaidia kumwona Yesu kuwa halisi zaidi,” anasema mwanamke mmoja. “Nimethamini jukumu lake. Ninataka kuwa na maisha yenye kusudi zaidi sasa na kushiriki katika habari njema ambayo wanadamu wanahitaji sana.”
Baba mmoja anaandika hivi: “Kitabu hicho kimenifanya nione umuhimu wa kuiga mfano mkamilifu tulioachiwa na Yesu . . . Katika kitabu hicho nimejifunza kutafakari mafundisho ya Yesu na sifa alizoonyesha alipokuwa duniani kama vile unyenyekevu, upendo, subira nyingi, utii, na ustahimilivu. Yesu alituachia mfano mzuri ambao umenitia moyo kufanya maendeleo.”
Msomaji mwingine alikubaliana kabisa na maneno yaliyo kwenye jalada la mwisho, ambayo yanasema hivi kwa sehemu: “Yesu Kristo ndiye Kiongozi ambaye tumepewa na Mungu, na kila mwanadamu anamhitaji. . . . Kitabu hiki kitakusaidia umjue Yesu vizuri zaidi na kumfuata kwa ukaribu zaidi.” Kisha msomaji huyo akasema, “Kwa kweli kitabu hicho kinatusaidia kumpenda Yesu, kumwamini, kumtii na kumfuata.”
Kitabu ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’ kina kurasa 192 zinazotia ndani kurasa nzima 13 zenye picha zinazoonyesha sehemu mbalimbali za maisha ya Yesu duniani. Unaweza kuomba kitabu hicho kwa kujaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Bila masharti, ningependa kupokea kitabu kilichoonyeshwa hapa.
□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.