“Ninahitaji Kufarijiwa”
● Ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova nchini Mexico ilipokea barua ifuatayo kutoka kwa mwanamke anayefanya kazi katika shule inayowatunza wasiojiweza na wenye matatizo ya akili. Aliandika hivi: “Mei tarehe 9, mama yangu mpendwa alikufa. Siwezi kueleza jinsi ninavyohisi. Miezi kadhaa kabla hajafa, nilifanya utafiti kazini kuhusu kifo na jinsi ya kushughulika na hisia zinazotokea mtu anapokufa. Nilifikiri ningefaidika kwa kufanya hivyo, lakini sikufaidika.”
Kisha, wakati mmoja mwanamke huyo alipokuwa na huzuni nyingi, alimwomba Mungu, akisema, “Ninahitaji kufarijiwa.” Anasema hivi, “Usiku huo, nilisoma broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. Nilihisi broshua hiyo ilikuwa ameandikwa kwa ajili yangu. Ilieleza kwamba ni sawa kulia. Chini ya kichwa ‘Naweza Kuishije Nikiwa na Huzuni Yangu?’ broshua hiyo inasema hivi: ‘Usipunguze umaana wa thamani ya sala. . . . Kwa kweli ule msaada ambao Mungu huandaa hufanya hali iwe tofauti. . . . Ni kweli, msaada wa kimungu hauondoi umivu, lakini waweza kufanya hali iwe rahisi zaidi kuvumilia. Hilo halimaanishi kwamba hutalia tena au utamsahau mpendwa wako. Lakini waweza kupata nafuu.’ Maneno hayo ni yenye faida.”
Ikiwa umempoteza mpendwa katika kifo na unahisi unahitaji kufarijiwa, huenda wewe au mtu unayejua akafarijika kwa kusoma broshua yenye kurasa 32 Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa.
Unaweza kuomba broshua hiyo kwa kujaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Bila masharti, ningependa kupokea broshua iliyoonyeshwa hapa chini.
□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.