Utangulizi
Mara nyingi watu hawawaheshimu wengine, hivyo mtu anapoonyesha heshima jambo hilo huwashangaza sana watu.
Kwa mfano, watu wengi hawawaheshimu wazazi wao, wazee, polisi, waajiri, walimu, na watu kwa ujumla. Kwa kuongezea, ni kawaida kwa watu kuwakejeli wengine katika mitandao ya kijamii! Makala moja ya Harvard Business Review, ilisema kwamba “kuna ongezeko kubwa” la ukosefu wa heshima. Inaongezea kusema kwamba watu wengi “wanazidi kuwakosea wengine heshima, na wengi wameanza kutambua na kuathiriwa na hali hiyo.”