Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 22
  • Yusufu Anawekwa Katika Gereza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yusufu Anawekwa Katika Gereza
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Mtumwa Aliyemtii Mungu
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • “Je, Tafsiri Si za Mungu?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • “Ninawezaje Kufanya Ubaya Huu Mkubwa?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Yehova Anakusaidia Ili Ufanikiwe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 22
Yusufu akiwa gerezani

HADITHI YA 22

Yusufu Anawekwa Katika Gereza

YUSUFU ana miaka 17 tu anapopelekwa Misri. Anauzwa kwa Potifa. Potifa anafanya kazi ya mfalme wa Misri, anayeitwa Farao.

Yusufu anafanya kazi ya bwana wake, Potifa, kwa bidii. Kwa nini Yusufu amewekwa humu ndani ya gereza? Ni kwa sababu ya mke wa Potifa.

Yusufu anakuwa mwanamume mwenye sura nzuri sana, mke wa Potifa anataka alale naye. Lakini Yusufu anajua hilo ni kosa, hawezi kulifanya. Mke wa Potifa anakasirika sana. Basi mume anaporudi nyumbani, anamwambia uongo na kusema: ‘Yusufu huyo mbaya alitaka kulala nami!’ Potifa anamwamini mke wake, naye anamkasirikia sana Yusufu. Basi anamtupa gerezani.

Upesi msimamizi wa gereza aona Yusufu ni mtu mzuri. Basi anamweka kuwa msimamizi wa wafungwa wengine wote. Baadaye Farao akamkasirikia mnyweshaji wake na mwokaji wake, na kuwatia gerezani. Usiku mmoja kila mmoja wao anaota ndoto ya pekee, lakini hawajui maana ya ndoto zao, kesho yake Yusufu anasema: ‘Niambieni ndoto zenu.’ Wanamwambia. Na kwa msaada wa Mungu, Yusufu anawaambia maana ya ndoto zao.

Kwa mnyweshaji, Yusufu anasema: Kwa siku tatu utafunguliwa utoke gerezani , uwe mnyweshaji wa Farao tena.’ Lakini kwa mwokaji, Yusufu anasema: ‘Katika siku tatu Farao atakukata kichwa chako.’

Katika muda wa siku tatu inakuwa kama Yusufu alivyosema. Farao anamkata kichwa mwokaji wake. Lakini mnyweshaji, anafunguliwa gerezani na kuanza kumtumikia mfalme tena. Lakini mnyweshaji huyo anamsahau Yusufu! Hamwambii Farao habari zake, naye Yusufu anaendelea kukaa gerezani.

Mwanzo 39:1-23; 40:1-23.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki