Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 25
  • Jamaa Inahama Kwenda Misri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jamaa Inahama Kwenda Misri
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Hakumsahau Yosefu Kamwe
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • “Je, Mimi Niko Mahali pa Mungu?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Yusufu Anachukiwa na Ndugu Zake
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • “Tafadhali Sikilizeni Ndoto Hii”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 25
Yakobo na Yusufu waungana tena kwa shangwe huko Misri

HADITHI YA 25

Jamaa Inahama Kwenda Misri

YUSUFU hawezi kujizuia tena. Anawaambia watumishi wake wote waondoke chumbani. Anapokuwa peke yake pamoja na ndugu zake, Yusufu anaanza kulia. Twaweza kuwazia jinsi ndugu zake wanavyoshangaa, kwa sababu hawajui sababu analia. Mwishowe anawaambia hivi: ‘Mimi ni Yusufu. Je! baba yangu angali hai?

Ndugu zake wanashangaa sana hata hawawezi kusema. Wanaogopa. Lakini Yusufu anawaambia hivi: ‘Tafadhali njoni karibu zaidi.’ Wanapokaribia zaidi, anawaambia hivi: ‘Mimi ni ndugu yenu Yusufu, ambaye mliuza Misri.’

Yusufu anaendelea kusema kwa huruma hivi: ‘Msijilaumu kwa sababu mliniuza huku. Ni Mungu aliyenituma nije Misri niokoe maisha za watu. Farao amenifanya niwe mtawala wa nchi yote. Basi sasa fanyeni haraka mrudi kwa baba yangu mkamwambie hivyo. Mwambieni aje kukaa huku.’

Kisha Yusufu anawakumbatia ndugu zake, na kuwabusu wote. Farao anaposikia kwamba ndugu za Yusufu wamekuja anamwambia Yusufu hivi: ‘Na wachukue magari waende kumchukua baba na jamaa zao warudi huku. Nitawapa nchi iliyo bora zaidi katika Misri yote.’

Ndivyo walivyofanya. Hata unaweza kumwona Yusufu akimlaki baba yake anapofika Misri akiwa na jamaa yake yote.

Ndugu za Yusufu na familia zao wanahamia Misri

Jamaa ya Yakobo imekuwa kubwa sana. Walipohama kwenda Misri wote walikuwa 70, kutia Yakobo na watoto wake na wajukuu wake. Lakini walikuwako pia wake, na labda watumishi wengi. Wote hao wakahama kwenda Misri. Wakaitwa Waisraeli, kwa sababu Mungu alikuwa amebadili jina la Yakobo kuwa Israeli. Waisraeli wakawa watu wa pekee sana kwa Mungu kama tutakavyoona baadaye.

Mwanzo 45:1-28; 46:1-27.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki