Furahia Milele Maisha Duniani!
Kitabu hiki kidogo kimepigwa chapa kukusaidia kujua ni nani aliumba dunia na vitu vyote vilivyo duniani. Utapata habari kwamba Mungu, ambaye aliumba dunia, ana jina lake. Katika kitabu hiki kidogo tutaeleza pia sababu iliyofanya Mungu aumbe mwanadamu na namna wewe unaweza kufurahia milele maisha duniani.
Sisi tunatumaini kwamba picha hizi nyingi zitakusaidia ufikirie mambo haya kwa njia nzuri zaidi. Ili upate faida kubwa zaidi, inafaa usome maandiko ya Biblia ambayo yameonyeshwa kando ya picha nyingi. Kwa njia hiyo utaweza kujisomea mwenyewe nyingine za ahadi nzuri za Mungu ambazo zimo ndani ya Biblia na mambo ambayo Mungu anasema wewe ufanye ili utimiziwe ahadi hizo.
Unaweza pia kutumia kitabu hiki kidogo kusaidia wengine. Ikiwa una watoto, unaweza kukitumia kuwasaidia wajue habari za Mungu. Ikiwa unaishi katika nchi ambako watu wengi hawajui kusoma, unaweza kutumia picha kuwasaidia kufahamu makusudi ya Mungu ili wao pia waweze kusaidia jirani zao.
Sisi tunatumaini kwa moyo mweupe kwamba kujifunza habari hizi kutakufungulia njia ya kupata baraka nyingi, hata uone vile unaweza kuishi milele hapa duniani.