“Endelea Katika Mambo Yale Ambayo Ulijifunza”
Hivyo ndivyo mtume Paulo alivyomwandikia Timotheo kijana. (2 Timotheo 3:14, NW) Baada ya kusoma kichapo hiki, unajua mambo mema mengi ambayo Mungu amewekea akiba wale wanaompenda. Lakini unahitaji uzidi kufanya maendeleo katika njia ya kiroho. Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia, ikiwa hujaanza kupokea msaada huo. Wewe andikia tu Mashahidi wa Yehova kwenye anwani inayofaa iliyoorodheshwa hapa chini, uombe habari zaidi au kwamba mmoja wa Mashahidi wa Yehova aje nyumbani kwako na kujifunza Biblia pamoja na wewe kwa ukawaida bila malipo.