Jinsi ya Kutumia Broshua Hii
Kusudi la broshua hii ni ili kujifunza Biblia. Inapasa itumiweje? Twadokeza programu ifuatayo: Mwanzoni mwa kila somo, kuna maswali. Katika mabano baada ya kila swali, utapata nambari za mafungu ambamo majibu yanapatikana. Soma maswali yote kwanza. Yafikirie. Kisha usome kila fungu, na kuyachunguza maandiko katika Biblia yako. Unapomaliza somo, rudia maswali na ujaribu kukumbuka jibu la Biblia kwa kila swali. Unapomaliza broshua nzima, rudia mwanzo na upitie maswali yote.