Utangulizi
Msomaji Mpendwa:
‘Njoo uwe mfuasi wangu.’ (Marko 10:21) Huo ni mwaliko kutoka kwa Yesu Kristo. Anatualika tumfuate. Je, utaukubali mwaliko huo? Kufanya hivyo kutakuwa na matokeo makubwa sana maishani mwako. Kwa nini?
Yehova alimtuma Mwana wake mzaliwa-pekee duniani ili autoe uhai wake kuwa fidia. (Yohana 3:16) Mbali na kufa kwa ajili yetu, Mwana huyo alituwekea kielelezo, au mfano wa kufuata maishani. Katika kila jambo alilofanya, alidumisha utimilifu na kuufanya moyo wa Baba yake ushangilie. Pia, Yesu alituonyesha jinsi tunavyoweza kumwiga Baba yake. Kupitia maneno na matendo yake, Mwana huyo alionyesha kikamilifu njia na mapenzi ya Baba yake.—Yohana 14:9.
Biblia inasema kwamba Yesu alituachia ‘kielelezo ili tufuate hatua zake kwa ukaribu.’ (1 Petro 2:21) Ikiwa tunataka kumkaribia Yehova zaidi, ikiwa tunataka kuwa na maisha yenye kusudi sasa, na ikiwa tunataka kubaki katika barabara inayoelekea kwenye uzima wa milele, lazima tufuate hatua za Kristo kwa ukaribu.
Ili kuanza safari hiyo, tunahitaji kujifunza kuhusu maisha ya Yesu duniani. Kwa hiyo, inafaa tujifunze kwa makini habari zilizo katika Biblia kumhusu Yesu. Kutafakari mambo ambayo Yesu alisema na kufanya na kufikiria jinsi tunavyoweza kumwiga katika maneno na matendo yetu, kutatusaidia kuona waziwazi jinsi tunavyoweza kumfuata.
Kitabu hiki na kikusaidie kumpenda Yesu na Yehova zaidi. Nao upendo huo ukuchochee kufuata hatua za Yesu kwa ukaribu ili uufanye moyo wa Yehova ushangilie sasa na milele.
Wachapishaji