Ungependa Kujua Mengi Zaidi?
Broshua hii inatoa muhtasari mfupi wenye kusisimua wa ujumbe ulio katika Biblia. Hata hivyo, kusudi lake si kueleza kirefu mambo ambayo Biblia inafundisha kuhusu kila jambo.
Kwa mfano, huenda ungependa kupata majibu ya Biblia kuhusu maswali kama haya: Je, kweli Mungu ananijali? Inakuwaje tunapokufa? Ninaweza kupata furaha maishani jinsi gani?
Majibu ya maswali hayo na mengine yenye kusisimua yanaweza kupatikana katika kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Kitabu hicho kimekusudiwa kuwasaidia watu kujifunza Biblia hatua kwa hatua. Kujifunza kwa njia hiyo kunamsaidia mtu kuunganisha mistari mbalimbali ya Biblia inayozungumzia habari fulani hususa. Unaweza kuomba nakala ya kitabu hicho kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani ifaayo iliyoonyeshwa hapa chini.
Unaweza kusoma au kuomba utembelewe au upakue chapisho hili kwenye tovuti ya www.jw.org.