Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jl somo la 3
  • Kweli za Biblia Zilifunuliwaje Tena?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kweli za Biblia Zilifunuliwaje Tena?
  • Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Habari Zinazolingana
  • “Mimi Nipo Pamoja Nanyi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Wakristo Huabudu kwa Roho na Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Uzima wa Milele Duniani—Tumaini Lililofunuliwa Tena
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Kumwiga Mungu wa Ukweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
Pata Habari Zaidi
Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
jl somo la 3

SOMO LA 3

Kweli za Biblia Zilifunuliwaje Tena?

Wanaume wakijifunza Biblia katika miaka ya 1870

Wanafunzi wa Biblia wa miaka ya 1870

Mwanamume akisoma nakala ya kwanza ya gazeti Mnara wa Mlinzi

Toleo la kwanza la Mnara wa Mlinzi, 1879

Mwanamke ameshika magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!

Mnara wa Mlinzi la wakati huu

Biblia ilitabiri kwamba baada ya kifo cha Kristo, walimu wa uwongo wangetokea miongoni mwa Wakristo wa mapema na kupotosha kweli za Biblia. (Matendo 20:29, 30) Baada ya muda, jambo hilo lilitukia. Walimu hao walichanganya mafundisho ya Yesu na mafundisho ya dini za kipagani, na hivyo Ukristo bandia ukatokea. (2 Timotheo 4:3, 4) Tunawezaje kuwa na uhakika kwamba leo tunaelewa kwa usahihi yale ambayo Biblia inafundisha hasa?

Wakati ulifika wa Yehova kufunua ukweli. Alitabiri kwamba ‘wakati wa mwisho ujuzi wa kweli ungekuwa mwingi.’ (Danieli 12:4) Mnamo 1870, kikundi kidogo cha watu waliokuwa wakitafuta ukweli kilitambua kwamba mafundisho mengi ya kidini hayakupatana na Maandiko. Kwa hiyo, walianza kufanya utafiti ili kuelewa mafundisho ya kweli ya Biblia, na Yehova akawasaidia kuelewa Maandiko.

Watu wanyoofu waliichunguza Biblia kwa makini. Wanafunzi hao wa Biblia waliotutangulia, walitumia njia ya kujifunza ambayo bado tunaitumia leo. Walizungumzia Biblia kwa kuchunguza jambo moja baada ya lingine. Waliposoma sehemu ya Biblia ambayo haikueleweka kwa urahisi, walichunguza maandiko mengine ili kuielewa. Walipofikia uamuzi uliopatana na Maandiko yote, waliandika jambo hilo. Kwa kuacha Biblia ijieleze yenyewe walifanikiwa kufunua tena ukweli kuhusu jina la Mungu na Ufalme wake, kusudi lake kuelekea wanadamu na dunia, hali ya wafu, na tumaini la ufufuo. Uchunguzi wao uliwaweka huru kutokana na mafundisho na desturi nyingi za uwongo.—Yohana 8:31, 32.

Kufikia mwaka wa 1879 Wanafunzi wa Biblia walitambua kwamba wakati ulikuwa umefika wa kutangaza kweli za Biblia kotekote. Basi, mwaka huo wakaanza kuchapisha gazeti la Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova, ambalo bado tunaendelea kulichapisha. Leo, tunawatangazia watu ujumbe wa kweli za Biblia katika nchi 240, tukitumia lugha 750 hivi. Leo, ujuzi wa kweli ni mwingi kuliko wakati mwingine wowote!

  • Ni nini kilichotokea kuhusiana na kweli za Biblia baada ya kifo cha Kristo?

  • Ni nini ambacho kimetusaidia kufunua tena ukweli ulio katika Neno la Mungu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki