Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jl somo la 7
  • Mikutano Yetu Hufanywaje?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Yetu Hufanywaje?
  • Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Habari Zinazolingana
  • Unaalikwa kwa Uchangamfu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Mikutano ‘Inayotuchochea Katika Upendo na Matendo Mazuri’
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Mikutano ya Mashahidi wa Yehova Inaweza Kukunufaishaje?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Kwa Nini Tunapaswa Kukutanika Pamoja kwa Ajili ya Ibada?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
Pata Habari Zaidi
Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
jl somo la 7

SOMO LA 7

Mikutano Yetu Hufanywaje?

Mkutano wa Mashahidi wa Yehova nchini New Zealand

New Zealand

Mkutano wa Mashahidi wa Yehova nchini Japani

Japani

Mvulana akisoma Biblia nchini Uganda

Uganda

Mashahidi wawili wakifanya onyesho kuhusu habari fulani ya Biblia nchini Lithuania

Lithuania

Sehemu kuu ya mikutano ya Wakristo wa karne ya kwanza ilikuwa kuimba, kusali, hali kadhalika kusoma na kuzungumzia Maandiko. Nayo haikuhusisha desturi za kidini. (1 Wakorintho 14:26) Hivyo ndivyo tunavyofanya mikutano yetu leo.

Mafundisho yanategemea Biblia na yanatunufaisha. Mwishoni mwa juma, kila kutaniko hukutana ili kusikiliza hotuba ya Biblia kuhusu jinsi Maandiko yanavyohusiana na maisha yetu na nyakati tunamoishi. Sote tunahimizwa kuambatana na msemaji anapokuwa akisoma Maandiko. Baada ya hotuba, kuna Funzo la “Mnara wa Mlinzi” kwa muda wa saa moja. Funzo hilo hutegemea makala ya toleo la funzo la Mnara wa Mlinzi, na wote wako huru kutoa maelezo. Mazungumzo hayo yanatusaidia kuona jinsi tunavyoweza kutumia mwongozo wa Biblia katika maisha yetu. Makutaniko zaidi ya 110,000 ulimwenguni hujifunza habari ileile.

Tunasaidiwa kuboresha ustadi wa kufundisha. Pia, katikati ya juma sisi hukusanyika kwa ajili ya mkutano wenye sehemu tatu unaoitwa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo ambao hutegemea habari zinazochapishwa kila mwezi katika Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu. Sehemu ya kwanza ya mkutano huo, Hazina za Neno la Mungu, hutusaidia kuelewa sura kadhaa za Biblia ambazo wote katika kutaniko wamezisoma mapema. Kisha, sehemu ya pili, Boresha Huduma Yako, huwa na maonyesho ya jinsi ya kuzungumzia Biblia na wengine. Mshauri hutoa maelezo mafupi yanayotusaidia kuboresha ustadi wetu wa kusoma au kuzungumza. (1 Timotheo 4:13) Sehemu ya mwisho, Maisha ya Mkristo, huzungumzia jinsi tunavyoweza kutumia kanuni za Biblia maishani. Ni sehemu ya mazungumzo ya maswali na majibu ambayo huboresha uelewaji wetu wa Biblia.

Utakapoanza kuhudhuria mikutano yetu, utafurahia kuona kwamba unaweza kujifunza mengi kuhusu Biblia.—Isaya 54:13.

  • Unaweza kutazamia kusikia mambo gani katika mikutano ya Mashahidi wa Yehova?

  • Ni mkutano gani unaofanywa kila juma ambao ungependa kuhudhuria?

PATA KUJUA MENGI ZAIDI

Soma baadhi ya habari zitakazozungumziwa katika mikutano michache inayofuata. Unaposoma, chunguza mambo unayojifunza katika Biblia ambayo yanaweza kukusaidia maishani.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki