Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jl somo la 15
  • Wazee Hulitumikia Kutaniko Jinsi Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wazee Hulitumikia Kutaniko Jinsi Gani?
  • Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi Ambavyo Kutaniko Limepangwa
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Wazee Wanaosimamia Vema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • “Lichungeni Kundi la Mungu Lililo Chini ya Uangalizi Wenu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • “Mwendelee Kuwachukua Watu wa Namna Hiyo Kuwa Wapendwa Wanaothaminika”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
jl somo la 15

SOMO LA 15

Wazee Hulitumikia Kutaniko Jinsi Gani?

Mzee akizungumza na washiriki wa kutaniko

Finland

Mzee akifundisha kutanikoni

Kufundisha

Wazee wakiwatia moyo washiriki wa kutaniko

Uchungaji

Mzee akihubiri hadharani

Kuhubiri

Hatuna makasisi wanaolipwa. Badala yake, kama ilivyokuwa kutaniko la Kikristo lilipoanzishwa, waangalizi wanaostahili huwekwa rasmi ili ‘walichunge kutaniko la Mungu.’ (Matendo 20:28) Wazee ni wanaume wakomavu kiroho ambao wanaongoza katika kutaniko na kulichunga, “si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari mbele za Mungu; si kwa kupenda pato lisilo la haki, bali kwa hamu.” (1 Petro 5:1-3) Wazee hufanya kazi gani kwa faida yetu?

Wanatuhangaikia na kutulinda. Wazee huongoza na kulinda kutaniko kiroho. Kwa kuwa wanatambua kwamba Mungu amewakabidhi jukumu zito, wazee hawapigi ubwana, badala yake, wanachangia hali nzuri na shangwe kati ya washiriki wa kutaniko. (2 Wakorintho 1:24) Kama vile mchungaji anavyomtunza kila kondoo kwa bidii, wazee hujitahidi kumjua kila mmoja katika kutaniko.—Methali 27:23.

Wanatufundisha jinsi ya kufanya mapenzi ya Mungu. Kila juma, wazee huongoza mikutano ya kutaniko ili kuimarisha imani yetu. (Matendo 15:32) Wanaume hao ambao wamejitoa kwa moyo wote huongoza katika kazi ya kutangaza habari njema, wakihubiri pamoja nasi na kutuzoeza aina mbalimbali za huduma.

Wanatutia moyo. Ili kututunza kiroho, wazee hututembelea nyumbani kwetu au kuzungumza nasi kwenye Jumba la Ufalme ili kutusaidia na kutufariji kwa kutumia Maandiko.—Yakobo 5:14, 15.

Mbali na majukumu yao katika kutaniko, wazee wengi hufanya kazi ili kujiruzuku na wanahitaji kushughulikia familia zao. Ndugu hao wenye bidii wanastahili heshima kutoka kwetu.—1 Wathesalonike 5:12, 13.

  • Wazee wa kutaniko hufanya kazi gani?

  • Wazee huonyesha jinsi gani kwamba wanapendezwa na kila mmoja wetu?

PATA KUJUA MENGI ZAIDI

Ni nani wanaostahili kutumikia? Maandiko yanataja sifa ambazo wazee na watumishi wa huduma wanahitaji kutimiza ili wastahili. Unaweza kusoma kuhusu sifa hizo katika 1 Timotheo 3:1-10, 12, na Tito 1:5-9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki