Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • od kur. 193-205
  • Sehemu ya 2: Maisha ya Kikristo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sehemu ya 2: Maisha ya Kikristo
  • Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • Je, ‘Unampenda Jirani Yako Kama Unavyojipenda’?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Ndoa
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Twatambuliwa kwa Mwenendo Wetu
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Jinsi ya Kufanikiwa Katika Ndoa ya Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
Pata Habari Zaidi
Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
od kur. 193-205

MASWALI KWA AJILI YA WALE WANAOTAKA KUBATIZWA

Sehemu ya 2: Maisha ya Kikristo

Kwa kujifunza Biblia, umepata ujuzi kuhusu yale ambayo Yehova anataka ufanye na jinsi ya kuishi kupatana na viwango vyake vya uadilifu. Ili uishi kupatana na mambo ambayo umejifunza, huenda ulihitaji kufanya mabadiliko kadhaa kuelekea mwenendo wako na mtazamo wako kuhusu maisha. Sasa, kwa kuwa umeazimia kuishi kupatana na viwango vya uadilifu vya Yehova, unaweza kumtolea utumishi unaokubalika ukiwa mhudumu wa habari njema.

Kuzungumzia maswali yafuatayo kutakusaidia kukazia akilini matakwa ya uadilifu ya Yehova na kukukumbusha baadhi ya mambo unayoweza kufanya ili uwe mtumishi wake anayekubalika. Habari hii itakazia umuhimu wa kufanya mambo yote ukiwa na dhamiri njema na kwa njia itakayomletea Yehova heshima.—2 Kor. 1:12; 1 Tim. 1:19; 1 Pet. 3:16, 21.

Tangu ulipoanza kujifunza Biblia mpaka sasa, ni wazi kwamba una hamu ya kujitiisha chini ya utawala wa Yehova na kuwa sehemu ya tengenezo lake. Maswali na marejeo ya Maandiko yatakusaidia kuchunguza ikiwa unaelewa maana ya kujitiisha chini ya mpango uliowekwa na Yehova, iwe ni katika kutaniko, familia, au inapohusu siasa za mfumo huu wa mambo. Bila shaka, utathamini sana mipango iliyowekwa na Yehova ya kuwaelimisha na kuwaimarisha watu wake kiroho. Mipango hiyo inatia ndani mikutano ya kutaniko ambayo unapaswa kuendelea kuhudhuria na kushiriki kadiri hali zako zinavyokuruhusu.

Kwa kuongezea, sehemu hii itazungumzia umuhimu wa kushiriki kwa ukawaida katika kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme ili kuwasaidia watu kumjua Yehova na mambo anayowafanyia wanadamu. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Mwishowe, sehemu hii itakusaidia kuona uzito wa wakfu wako kwa Yehova Mungu na ubatizo. Uwe na hakika kwamba Yehova anathamini utayari wako wenye unyoofu wa kukubali fadhili zisizostahiliwa anazokuonyesha.

1. Ndoa ya Kikristo inapaswa kufuata kigezo gani? Ni nini msingi pekee wa talaka ya Kimaandiko?

• “Je, hamkusoma kwamba yule aliyewaumba tangu mwanzo aliwaumba mwanamume na mwanamke na kusema: ‘Kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana na mke wake, na hao wawili watakuwa mwili mmoja’? Basi wao si wawili tena, bali mwili mmoja. Kwa hiyo, kile ambacho Mungu ameunganisha mtu yeyote asikitenganishe. . . . Yeyote anayemtaliki mke wake isipokuwa kwa sababu ya uasherati, na kumwoa mwingine, anafanya uzinzi.”—Mt. 19:4-6, 9.

2. Kwa nini wale wanaoishi pamoja kama mume na mke wanapaswa kuwa wameoana kisheria? Ikiwa umeoa au kuolewa, je, una hakika kwamba ndoa yako imeandikishwa kisheria serikalini?

• “Endelea kuwakumbusha wajitiishe na kuzitii serikali na mamlaka.”—Tito 3:1.

• “Ndoa na iheshimiwe kati ya wote, na kitanda cha ndoa kisiwe na unajisi, kwa maana Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.”—Ebr. 13:4.

3. Una jukumu gani katika familia?

• “Mwanangu, sikiliza nidhamu ya baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.”—Met. 1:8.

• “Mume ni kichwa cha mke wake kama vile Kristo alivyo kichwa cha kutaniko . .  Waume, endeleeni kuwapenda wake zenu, kama vile Kristo pia alivyolipenda kutaniko.”—Efe. 5:23, 25.

• “Akina baba, msiwe mkiwakasirisha watoto wenu, bali endeleeni kuwalea katika nidhamu na maagizo ya Yehova.”—Efe. 6:4.

• “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika kila jambo, kwa maana hilo humpendeza Bwana.”—Kol. 3:20.

• “Ninyi wake, jitiisheni kwa waume zenu.”—1 Pet. 3:1.

4. Kwa nini tunapaswa kuheshimu uhai?

• “[Mungu] huwapa watu wote uhai na pumzi na vitu vyote. . . . Kupitia kwake tuko hai, tunatembea, na tunaishi.”—Mdo. 17:25, 28.

5. Kwa nini hatupaswi kuua mtu yeyote, kutia ndani mtoto ambaye bado hajazaliwa?

• ‘Wanaume wakipambana na kumuumiza mwanamke mwenye mimba na kifo kitokee, basi ni lazima mlipe uhai kwa uhai.’—Kut. 21:22, 23.

• “Macho yako hata yaliniona nikiwa kiinitete; sehemu zake zote ziliandikwa katika kitabu chako kuhusiana na siku ambazo zingeumbwa, kabla sehemu yoyote haijakuwepo.”—Zab. 139:16.

• “Yehova anachukia . . . mikono inayomwaga damu isiyo na hatia.”—Met. 6:16, 17.

6. Sheria ya Mungu inasema nini kuhusu damu?

• “[Endeleeni] kujiepusha . . . na damu, na vitu vilivyonyongwa.”—Mdo. 15:29.

7. Kwa nini ni lazima tuwapende ndugu na dada zetu Wakristo?

• “Ninawapa ninyi amri mpya, kwamba mpendane; kama vile ambavyo nimewapenda, nanyi mpendane vivyo hivyo. Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu—mkiwa na upendo miongoni mwenu.”—Yoh. 13:34, 35.

8. Ili kuepuka kusambaza ugonjwa mbaya unaoambukiza: (a) Kwa nini mtu aliyeambukizwa hapaswi kuwakumbatia watu na kuwabusu? (b) Kwa nini hapaswi kukasirika ikiwa wengine hawatamkaribisha nyumbani kwao? (c) Kwa nini mtu ambaye huenda ameambukizwa na ugonjwa kama huo anapaswa kwenda kwa hiari kupima damu kabla ya kuanzisha uchumba? (d) Kwa nini mtu aliye na ugonjwa wa kuambukiza anapaswa kumwambia mratibu wa baraza la wazee kabla ya kubatizwa?

• “Msiwe na deni lolote kwa mtu yeyote, isipokuwa kupendana. . . . ‘Lazima umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.’ Upendo haumfanyii uovu jirani.”—Rom. 13:8-10.

• ‘Angalieni, si faida zenu wenyewe, bali pia faida za wengine.’—Flp. 2:4.

9. Kwa nini Yehova anatarajia tuwasamehe wengine?

• “Endeleeni kuvumiliana na kusameheana kwa hiari hata ikiwa yeyote ana sababu ya kulalamika juu ya mwingine. Kama vile Yehova alivyowasamehe kwa hiari, nanyi lazima mfanye vivyo hivyo.”—Kol. 3:13.

10. Utafanya nini ikiwa ndugu anakuchongea au kukupunja?

• “Ndugu yako akitenda dhambi, nenda ufunue kosa lake kati yako na yeye peke yenu. Akikusikiliza, umempata ndugu yako. Lakini asipokusikiliza, nenda pamoja na mtu mmoja au wawili, ili kwa ushahidi wa mashahidi wawili au watatu kila jambo lithibitishwe. Asipowasikiliza hao, liambie kutaniko. Asipolisikiliza kutaniko pia, na awe kwako kama mtu wa mataifa na kama mkusanya kodi.”—Mt. 18:15-17.

11. Yehova anahisije kuhusu dhambi zifuatazo:

▪ Uasherati

▪ Kutumia sanamu katika ibada

▪ Ngono kati ya watu wa jinsia moja

▪ Kuiba

▪ Kucheza kamari

▪ Ulevi

• “Msipotoshwe. Waasherati, waabudu-sanamu, wazinzi, wanaume wanaofanya ngono na wanaume, wezi, watu wenye pupa, walevi, watukanaji, na wanyang’anyi hawataurithi Ufalme wa Mungu.”—1 Kor. 6:9, 10.

12. Inapohusu uasherati, ambao unatia ndani matendo mbalimbali ya ngono nje ya ndoa, umeazimia kufanya nini?

• “Ukimbieni uasherati!”—1 Kor. 6:18.

13. Kwa nini tunapaswa kuepuka kutumia dawa zinazosababisha uraibu au zinazopumbaza akili kwa sababu isiyo ya matibabu?

• “[Toeni] miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, na yenye kukubalika kwa Mungu, utumishi mtakatifu pamoja na nguvu zenu za kufikiri. Na acheni kufinyangwa na mfumo huu wa mambo, bali mgeuzwe kwa kufanya upya akili yenu, ili mjihakikishie wenyewe mapenzi ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu.”—Rom. 12:1, 2.

14. Ni mazoea gani ya kuwasiliana na roho waovu ambayo Mungu anakataza?

• “Asipatikane miongoni mwenu . . . mtu yeyote anayefanya uaguzi, mtu yeyote anayefanya uchawi, mtu yeyote anayetafuta ishara za ubashiri, mlozi, mtu yeyote anayewafunga wenzake kwa uchawi, mtu yeyote anayetafuta ushauri kutoka kwa watu wanaowasiliana na roho, mpiga ramli, au mtu yeyote anayetafuta habari kuhusu wafu.”—Kum. 18:10, 11.

15. Mtu akitenda dhambi nzito na anataka kurudisha uhusiano mzuri na Yehova, anapaswa kufanya nini haraka iwezekanavyo?

• “[Niliungama] dhambi yangu kwako; sikufunika kosa langu. Nilisema: ‘Nitaungama makosa yangu kwa Yehova.’”—Zab. 32:5.

• “Je, kuna yeyote aliye mgonjwa kati yenu? Na awaite wazee wa kutaniko, nao wasali kwa ajili yake, wakimpaka mafuta katika jina la Yehova. Na sala ya imani itamponya huyo mgonjwa, na Yehova atamwinua. Pia, ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.”—Yak. 5:14, 15.

16. Ukijua kwamba Mkristo mwenzako amefanya dhambi nzito, unapaswa kufanya nini?

• “Ikiwa mtu amesikia mwito wa hadharani wa kutoa ushahidi kuhusu jambo ambalo amejionea au kusikia au kujua, lakini amekataa kutoa habari, basi ametenda dhambi, naye atawajibika kwa sababu ya kosa lake.”—Law. 5:1.

17. Tangazo likitolewa kwamba mtu fulani si Shahidi wa Yehova tena, tunapaswa kumtendea jinsi gani?

• “[Acheni] kushirikiana na mtu yeyote anayeitwa ndugu ambaye ni mwasherati au mtu mwenye pupa au anayeabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi, hata msile chakula pamoja na mtu wa namna hiyo.”—1 Kor. 5:11.

• “Mtu yeyote akija kwenu naye haleti fundisho hili, msimpokee nyumbani mwenu wala kumsalimu.”—2 Yoh. 10.

18. Kwa nini marafiki wako wa karibu wanapaswa kuwa watu wanaompenda Yehova?

• “Anayetembea na wenye hekima atakuwa na hekima, lakini anayeshirikiana na wapumbavu ataumia.”—Met. 13:20.

• “Msipotoshwe. Kushirikiana na watu wabaya huharibu tabia nzuri.”—1 Kor. 15:33.

19. Kwa nini Mashahidi wa Yehova hawajihusishi na siasa?

• “Wao si sehemu ya ulimwengu, kama vile ambavyo mimi [Yesu] si sehemu ya ulimwengu.”—Yoh. 17:16.

20. Kwa nini unapaswa kutii mamlaka za serikali?

• “Kila mtu na ajitiishe kwa mamlaka zilizo kubwa, kwa maana hakuna mamlaka isipokuwa kupitia Mungu; mamlaka zilizopo zimewekwa na Mungu katika vyeo vyao vya kadiri.”—Rom. 13:1.

21. Ikiwa sheria fulani ya mwanadamu inapingana na sheria ya Mungu, utafanya nini?

• “Lazima tumtii Mungu kuwa mtawala badala ya wanadamu.”—Mdo. 5:29.

22. Ni maandiko gani yanayoweza kukusaidia kujitenga na ulimwengu unapochagua kazi ya kimwili?

• “Taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe.”—Mika 4:3.

• “Tokeni kwake [Babiloni Mkubwa], watu wangu, ikiwa hamtaki kushiriki pamoja naye dhambi zake, na ikiwa hamtaki kupokea sehemu ya mapigo yake.”—Ufu. 18:4.

23. Ni aina gani ya burudani na tafrija utakazochagua, na ni zipi utakazoepuka?

• “Yehova . . . humchukia mtu yeyote anayependa ukatili.”—Zab. 11:5.

• “Chukieni maovu; shikamaneni na mema.”—Rom. 12:9.

• “Mambo yoyote yaliyo ya kweli, mambo yoyote yaliyo ya hangaiko zito, mambo yoyote yaliyo ya uadilifu, mambo yoyote yaliyo safi kiadili, mambo yoyote yanayopendeka, mambo yoyote yanayosemwa vema, mambo yoyote ya wema wa adili, na mambo yoyote yanayostahili sifa, endeleeni kuyafikiria mambo hayo.”—Flp. 4:8.

24. Kwa nini Mashahidi wa Yehova hawashirikiani na dini nyingine katika ibada?

• “Hamwezi kuwa mkishiriki ‘meza ya Yehova’ na meza ya roho waovu.”—1 Kor. 10:21.

• “‘Mjitenge,’ asema Yehova, ‘na mwache kugusa kitu kichafu’; ‘nami nitawakaribisha ndani.’”—2 Kor. 6:17.

25. Ni kanuni zipi zitakazokusaidia kuamua ikiwa utasherehekea sherehe fulani au la?

• “Walichangamana na mataifa hayo na kuzikubali njia zao. Waliendelea kuabudu sanamu zao, nazo zikawa mtego kwao.”—Zab. 106:35, 36.

• “Waliokufa hawajui jambo lolote kamwe.”—Mhu. 9:5.

• “Wao si sehemu ya ulimwengu, kama vile ambavyo mimi si sehemu ya ulimwengu.”—Yoh. 17:16.

• “Wakati uliopita uliwatosha kufanya mapenzi ya mataifa, mlipofanya vitendo vya mwenendo mpotovu, uchu, kunywa kupita kiasi, karamu zenye vurugu, mashindano ya kunywa, na ibada za sanamu zenye kuchukiza.”—1 Pet. 4:3.

26. Masimulizi yaliyo katika Biblia yatakusaidiaje inapohusu kusheherekea siku ya kuzaliwa?

• “Siku ya tatu ilikuwa sikukuu ya kuzaliwa kwa Farao, kwa hiyo aliwafanyia karamu watumishi wake wote, akamtoa gerezani msimamizi mkuu wa vinywaji na mwokaji mkuu, akawaleta mbele ya watumishi wake. Akamrudisha msimamizi mkuu wa vinywaji kwenye cheo chake . . . Lakini akamtundika mwokaji mkuu.”—Mwa. 40:20-22.

• “Wakati wa sherehe ya sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, binti ya Herodia alicheza dansi na kumfurahisha sana Herode hivi kwamba akaahidi kwa kiapo kumpa chochote ambacho angeomba. Ndipo yule binti, akichochewa na mama yake, akasema: ‘Nipe kwenye sinia kichwa cha Yohana Mbatizaji.’ Basi akawatuma watu gerezani, nao wakamkata Yohana kichwa.”—Mt. 14:6-8, 10.

27. Kwa nini ungependa kufuata mwongozo wa wazee?

• “Watiini wale wanaoongoza kati yenu na mnyenyekee, kwa maana wanaendelea kuwalinda ninyi kama wale watakaotoa hesabu, ili wafanye hivyo kwa shangwe na si kwa huzuni, kwa maana kufanya hivyo kungewadhuru ninyi.”—Ebr. 13:17.

28. Kwa nini ni muhimu kwako na kwa familia yako kutenga wakati wa kusoma na kujifunza Biblia kwa ukawaida?

• “Anapendezwa na sheria ya Yehova, naye huisoma sheria Yake kwa sauti ya chini mchana na usiku. Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, mti unaozaa matunda katika majira yake, na majani yake hayanyauki. Na kila jambo analofanya litafanikiwa.”—Zab. 1:2, 3.

29. Kwa nini unapenda kuhudhuria na kushiriki katika mikutano?

• “Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kutaniko nitakusifu.”—Zab. 22:22.

• “Acheni tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri, bila kuacha kukutana pamoja, kama wengine walivyo na desturi, bali tutiane moyo, na kufanya hivyo zaidi kwa kadiri mnavyoona siku ile ikikaribia.”—Ebr. 10:24, 25.

30. Ni kazi gani muhimu zaidi ambayo Yesu ametupatia?

• “Nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, mkiwabatiza . . . , na kuwafundisha kushika mambo yote niliyowaamuru.”—Mt. 28:19, 20.

31. Tunapotoa michango kwa ajili ya kazi ya Ufalme au kuwasaidia ndugu na dada zetu, ni mtazamo gani ambao humpendeza Yehova?

• “Mheshimu Yehova kwa vitu vyako vyenye thamani.”—Met. 3:9.

• “Kila mmoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si kwa kutopenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda mtoaji mchangamfu.”—2 Kor. 9:7.

32. Wakristo wanatazamia kupatwa na hali zipi ngumu?

• “Wenye furaha ni wale ambao wameteswa kwa ajili ya uadilifu, kwa kuwa Ufalme wa mbinguni ni wao. Wenye furaha ni ninyi, watu wanapowashutumu na kuwatesa na kuwasingizia kila aina ya uovu kwa sababu yangu. Furahini na kushangilia sana, kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni, kwa maana hivyo ndivyo walivyowatesa manabii waliokuwapo kabla yenu.”—Mt. 5:10-12.

33. Kwa nini ni pendeleo la pekee kubatizwa ili kuwa Shahidi wa Yehova?

• “Neno lako likawa furaha na shangwe ya moyo wangu, kwa maana nimeitwa kwa jina lako, Ee Yehova Mungu.”—Yer. 15:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki