Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 41 uku. 100-uku. 101 fu. 2
  • Daudi na Sauli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Daudi na Sauli
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Sababu Yampasa Daudi Akimbie
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Daudi Anafanywa Mfalme
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • “Kutii Ni Bora Kuliko Dhabihu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • 1 Samweli—Yaliyomo
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 41 uku. 100-uku. 101 fu. 2
Daudi akizungumza kwa sauti akiwa juu ya mlima umbali fulani kutoka kwenye kambi ya Sauli

SOMO LA 41

Daudi na Sauli

Baada ya Daudi kumuua Goliathi, Mfalme Sauli alimweka Daudi asimamie jeshi lake. Daudi alishinda vita vingi, naye alijulikana na kusifiwa na watu wengi. Wakati wowote ambapo Daudi alirudi nyumbani, wanawake wangetoka nje wakicheza dansi na kuimba: ‘Sauli amepiga maelfu yake, na Daudi amepiga makumi ya maelfu yake!’ Sauli alianza kumwonea Daudi wivu na akataka kumuua.

Daudi alijua kupiga kinubi vizuri sana. Siku moja Daudi alipokuwa akipiga kinubi, Sauli alimrushia mkuki. Daudi akakwepa kabla tu ya mkuki kumpata nao ukapiga ukuta. Baada ya hapo, Sauli akajaribu mara nyingi zaidi kumuua Daudi. Mwishowe, Daudi akakimbia na kujificha nyikani.

Daudi akichukua mkuki wa Sauli huku Sauli akiwa amelala

Sauli akachukua jeshi la watu 3,000 na kwenda kumwinda Daudi. Sauli akaingia ndani ya pango ambamo Daudi na wanaume wake walikuwa wakijificha. Wanaume hao wakamwambia Daudi kwa sauti ya chini: ‘Hii ndiyo nafasi yako ya kumuua Sauli.’ Daudi akamnyemelea Sauli na kukata koti lake. Sauli hakutambua. Baadaye, Daudi akahisi vibaya kwa sababu alikuwa amemvunjia heshima mfalme mtiwa-mafuta wa Yehova. Hakuwaruhusu wanaume wake wamshambulie Sauli. Hata alimwambia Sauli kwamba alikuwa amepata nafasi ya kumuua lakini hakufanya hivyo. Je, Sauli angebadili nia yake kumwelekea Daudi?

Hapana. Sauli aliendelea kumwinda Daudi. Usiku mmoja Daudi na mpwa wake Abishai waliingia kimyakimya kwenye kambi ya Sauli. Hata Abneri, mlinzi wa Sauli, alikuwa amelala. Abishai akasema: ‘Hii ndiyo nafasi yetu! Niruhusu nimuue.’ Daudi akajibu: ‘Yehova atamwadhibu Sauli. Acha tuchukue mkuki wake na gudulia lake la maji tuondoke.’

Daudi akapanda juu ya mlima uliokuwa karibu na kambi ya Sauli. Akasema kwa sauti kubwa: ‘Abneri, kwa nini hukumlinda mfalme? Uko wapi mkuki wa Sauli na gudulia lake la maji?’ Sauli akatambua sauti ya Daudi na kusema: ‘Ungeweza kuniua, lakini hukufanya hivyo. Ninajua kwamba utakuwa mfalme anayefuata wa Israeli.’ Sauli akarudi kwenye jumba lake la kifalme. Lakini si wote katika familia ya Sauli waliomchukia Daudi.

“Ikiwezekana, kwa kadiri inavyowategemea ninyi, fanyeni amani na watu wote. Wapendwa, msijilipizie kisasi bali iachieni nafasi ghadhabu.”​—Waroma 12:18, 19

Maswali: Kwa nini Sauli alitaka kumuua Daudi? Kwa nini Daudi alikataa kumuua Sauli?

1 Samweli 16:14-23; 18:5-16; 19:9-12; 23:19-29; 24:1-15; 26:1-25

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki