Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 54 uku. 130-uku. 131 fu. 1
  • Yehova Alimwonyesha Yona Subira

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yehova Alimwonyesha Yona Subira
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Alijifunza Kuwa Mwenye Rehema
    Igeni Imani Yao
  • Alijifunza Kuwa Mwenye Rehema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Kitabu Cha Biblia Namba 32—Yona
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Yona Ajifunza Juu ya Rehema ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 54 uku. 130-uku. 131 fu. 1
Yona anazama baharini huku samaki mkubwa akimkaribia

SOMO LA 54

Yehova Alimwonyesha Yona Subira

Watu katika jiji la Ashuru lililoitwa Ninawi walikuwa waovu. Yehova alimwambia nabii Yona aende Ninawi akawaonye kwamba wanapaswa kubadilika. Lakini Yona akakimbia kuelekea upande mwingine. Akaingia katika meli iliyokuwa ikielekea Tarshishi na kuanza safari.

Meli hiyo ilipokuwa baharini, dhoruba kali ikaanza kuvuma, nao mabaharia wakaogopa sana. Wakasali kwa miungu yao na kuuliza: ‘Kwa nini hali hii inatokea?’ Mwishowe, Yona akawaambia hivi: ‘Mimi ndiye ninayepaswa kulaumiwa. Ninakimbia ili nisifanye kile ambacho Yehova aliniambia nifanye. Nitupeni baharini, na bahari itatulia.’ Mabaharia hawakutaka kumtupa Yona baharini, lakini akasisitiza wamtupe. Walipomtupa baharini, dhoruba ikatulia.

Yona alifikiri kwamba atakufa. Alipokuwa akizama zaidi na zaidi, akasali kwa Yehova. Kisha Yehova akamtuma samaki mkubwa sana. Samaki huyo akammeza Yona, lakini hakumuua. Akiwa ndani ya samaki huyo, Yona alisali hivi: ‘Ninaahidi kwamba sikuzote nitakutii.’ Yehova akamlinda Yona ndani ya samaki huyo kwa siku tatu, kisha akamfanya samaki huyo amtapike kwenye nchi kavu.

Kwa kuwa Yehova alikuwa amemwokoa Yona, je, hilo lilimaanisha kwamba hakuhitaji kwenda Ninawi? La. Kwa mara nyingine tena Yehova akamwambia Yona aende Ninawi. Pindi hii Yona alitii. Alienda na kuwaambia watu hao waovu hivi: ‘Baada ya siku 40, Ninawi litaangamizwa.’ Lakini jambo lisilotazamiwa likatokea. Watu wa Ninawi wakasikiliza na kubadili njia zao. Mfalme wa Ninawi akawaambia watu wake hivi: ‘Mwiteni Mungu, na mtubu. Labda atabadili mawazo yake na hatatuangamiza.’ Yehova alipoona kwamba watu walikuwa wametubu, hakuliangamiza jiji la Ninawi.

Yona anakaribia Ninawi

Yona akakasirika kwamba jiji hilo halikuwa limeangamizwa. Hebu fikiria: Yehova alikuwa amemwonyesha Yona subira na rehema, lakini Yona hakutaka kuwaonyesha rehema watu wa Ninawi. Badala yake, akaketi nje ya jiji chini ya kivuli cha mmung’unye na kununa. Kisha mmea huo ukafa, naye Yona akakasirika. Kwa hiyo, Yehova akamwambia hivi: ‘Unaupenda mmea huu kuliko unavyowapenda watu wa Ninawi. Mimi niliwaonyesha rehema, nao wakaokoka.’ Alikuwa akimfundisha nini? Watu wa Ninawi walikuwa muhimu kuliko mmea wowote ule.

“Yehova . . . ni mwenye subira kwenu kwa sababu hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.”​—2 Petro 3:9

Maswali: Yehova alimfundisha Yona mambo gani? Tunaweza kujifunza nini kutokana na mambo yaliyompata Yona?

Yona 1:1–4:11

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki