Watoto; Vijana
Maoni ya Mungu kuhusu watoto
Yehova anaonyeshaje kwamba watoto na vijana wana thamani kwake?
Kum 6:6, 7; 14:28, 29; Zb 110:3; 127:3-5; 128:3, 4; Yak 1:27
Tazama pia Ayu 29:12; Zb 27:10; Met 17:6
Tazama pia “Familia”
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mwa 1:27, 28—Yehova anafanya kupata watoto kuwa sehemu muhimu ya kusudi lake la awali la kuijaza dunia
Mwa 9:1—Kupata watoto kunakuwa sehemu muhimu ya kutimiza amri ya Mungu ya kuijaza dunia baada ya Gharika
Mwa 33:5—Yakobo, mzee wa ukoo mwaminifu anaona watoto wake kuwa ishara ya kuwa na kibali cha Mungu
Mk 10:13-16—Yesu anamwiga Baba yake kwa kuwapenda watoto
Yehova anahisije kuhusu wale wanaowatesa au kuwatendea vibaya watoto?
Ni kanuni gani za Biblia zinazoonyesha kwamba watoto hawapaswi kubeba majukumu ya watu wazima?
Simulizi la Biblia linalohusika:
Mwa 33:12-14—Yakobo anatambua kwamba watoto wake hawawezi kutembea haraka kama watu wazima
Je, Mungu anapaswa kulaumiwa kwa sababu ya mateso wanayokabili watoto katika ulimwengu huu?
Yehova anatupatia uhakikisho gani kwamba mateso wanayokabili vijana na wazee yatakwisha?
Je, mfano mbaya wa wazazi au kutendewa vibaya utotoni kunafanya mtu awe hana thamani au afanye makosa yaleyale ambayo wazazi wake walifanya?
Tazama pia Kum 30:15, 16
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
2Fa 18:1-7; 2Nya 28:1-4—Hezekia anakuwa mfalme mkuu na mwaminifu, licha ya kulelewa na baba mwovu aliyewaua baadhi ya watoto wake mwenyewe
2Fa 21:19-26; 22:1, 2—Yosia anakuwa mfalme wa pekee, licha ya kulelewa na Amoni, baba yake, aliyekuwa mwovu
1Ko 10:11, 12—Mtume Paulo anaeleza kwamba tunaweza kujifunza kutokana na makosa ya wengine na kuamua kutofanya makosa hayo
Flp 2:12, 13—Mtume Paulo anatukumbusha kwamba tunahitaji kuufanyia kazi wokovu wetu
Majukumu ya watoto na vijana
Yehova anawaonaje watoto ambao bado wanaishi nyumbani kwa wazazi wanaomwogopa Mungu?
Simulizi la Biblia linalohusika:
Mwa 19:12, 15—Sababu moja inayofanya mabinti wa Loti walindwe na malaika ni uadilifu wa baba yao
Ikiwa wazazi wana uhusiano mzuri na Mungu, je ni lazima watoto wao pia wawe na uhusiano mzuri na Mungu?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Law 10:1-3, 8, 9—Inawezekana kwamba watoto wa Kuhani Mkuu Haruni wanauawa kwa sababu ya ulevi
1Sa 8:1-5—Ingawa Samweli ni nabii mwadilifu, watoto wake si wanyoofu
Watoto wanaotaka kibali cha Mungu wanahitaji kufanya nini?
Kwa nini vijana wanapaswa kuhudhuria mikutano ya kutaniko?
Kum 31:12, 13; Ebr 10:24, 25
Simulizi la Biblia linalohusika:
Mt 15:32-38—Watu wanaomsikiliza Yesu wanatia ndani watoto
Kwa nini inafaa watoto wamwabudu Mungu?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
1Sa 17:4, 8-10, 41, 42, 45-51—Yehova anamtumia kijana Daudi kutetea jina Lake kwa kumshinda yule jitu katili
2Fa 5:1-15—Yehova anamtumia msichana Mwisraeli kumsaidia mkuu wa jeshi asiye Mwisraeli ajifunze kumhusu Mungu wa kweli
Mt 21:15, 16—Yesu anathamini jitihada za watoto za kumsifu Masihi
Mungu anawaonaje watoto wa wazazi wasio waamini?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Hes 16:25, 26, 32, 33—Baadhi ya watu wanapomwasi Musa na Haruni, Yehova anawaadhibu watu hao na watu wa familia zao wanaowaunga mkono
Hes 26:10, 11—Ingawa Kora aliyeasi aliangamizwa, watoto wake waliokolewa, inaelekea ni kwa sababu ya uaminifu wao
Kwa nini vijana leo wanapaswa kuchagua marafiki kwa hekima?
Tazama pia 2Ti 3:1-5
Vijana Wakristo wanapaswa kutafuta marafiki wa aina gani?
Tazama pia “Kushirikiana na Wengine”