Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • scl kur. 107-109
  • Uvumilivu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uvumilivu
  • Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
scl kur. 107-109

Uvumilivu

Je, watumishi wa Yehova wanahitaji uvumilivu?

1Ko 13:​4, 7; 1Ti 6:11; 2Pe 1:​5, 6

Kwa nini tunapaswa kutarajia kwamba baadhi ya watu watatupuuza au kututesa tunapowahubiria?

Mt 10:22; Yoh 15:​18, 19; 2Ko 6:​4, 5

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 2Pe 2:5; Mwa 7:23; Mt 24:​37-39—Ingawa Noa ni “mhubiri wa uadilifu,” watu wengi wanakataa ujumbe wake, hivyo yeye na familia yake tu ndio wanaookoka wakati wa Gharika

    • 2Ti 3:​10-14—Mtume Paulo anatumia mfano wake wa uvumilivu kumtia moyo Timotheo avumilie

Kwa nini tunaweza kutarajia upinzani hata kutoka kwa watu wa familia yetu?

Mt 10:​22, 36-38; Lu 21:​16-19

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mwa 4:​3-11; 1Yo 3:​11, 12—Kaini anamuua ndugu yake kwa sababu matendo ya Kaini ni maovu, na matendo ya Abeli ni ya uadilifu

    • Mwa 37:​5-8, 18-28—Ndugu za Yosefu wanamshambulia na kumuuza Yosefu awe mtumwa baada ya kuwasimulia ndoto kutoka kwa Yehova

Tunapoteswa, kwa nini hatuhitaji kuogopa kifo?

Mt 10:28; 2Ti 4:​6, 7

Tazama pia Ufu 2:10

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Da 3:​1-6, 13-18—Shadraki, Meshaki, na Abednego hawakuabudu sanamu ingawa mfalme alisema kwamba wangeuawa ikiwa wangekataa kuabudu sanamu

    • Mdo 5:​27-29, 33, 40-42—Licha ya tishio la kuuawa, mitume wanaendelea kuhubiri kwa uvumilivu

Ni nini kitakachotusaidia kuendelea kuwa waaminifu kwa Yehova hata tunapotiwa nidhamu?

Met 3:​11, 12; Ebr 12:​5-7

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Hes 20:​9-12; Kum 3:​23-28; 31:​7, 8—Nidhamu ya Yehova inamvunja moyo nabii Musa; hata hivyo, anavumilia kwa uaminifu hadi mwisho

    • 2Fa 20:​12-18; 2Nya 32:​24-26—Mfalme Hezekia anatenda dhambi, nabii wa Yehova anamrekebisha, na kwa unyenyekevu anakubali nidhamu na kuendelea kumtumikia Yehova

Kwa nini inaweza kuwa vigumu kuvumilia wengine wanapoacha kumtumikia Yehova?

Yer 1:​16-19; Hab 1:​2-4

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Zb 73:​2-24—Mtunga zaburi anapoona amani na ufanisi wa watu waovu, anatilia shaka thamani ya kuvumilia katika utumishi wake kwa Yehova

    • Yoh 6:​60-62, 66-68—Ingawa watu wengi wanaacha kumfuata Yesu, mtume Petro anaazimia kuendelea kumfuata Yesu

Ni nini kitakachotusaidia kuvumilia?

Kushikamana na Yehova

Kum 30:​19, 20; Ro 15:​5, 6; 1Ko 10:13

Kupata ujuzi wa Neno la Mungu kupitia kujifunza na kutafakari

Mhu 7:12; Ro 15:4; Kol 1:​10, 11; 2Pe 3:​15-18

Kumkaribia Yehova kwa ukawaida kupitia sala za kutoka moyoni

Ro 12:12; Kol 4:2; 1Pe 4:7

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Da 6:​4-11—Nabii Danieli anaendelea kusali bila kujificha na kwa ukawaida, licha ya kwamba kufanya hivyo kungehatarisha uhai wake

    • Mt 26:​36-46; Ebr 5:7—Katika usiku wa mwisho wa maisha yake hapa duniani, Yesu anasali kwa bidii na kuwatia moyo wengine wafanye hivyo

Kushirikiana kwa ukawaida na waabudu wenzetu katika ibada

Ro 1:​11, 12; Ebr 10:​23-25

Kufikiria kuhusu baraka ambazo Yehova ametuahidi

Ro 8:25; 1Th 1:3; Ebr 11:6; 12:​1, 2

Kuimarisha upendo wetu kwa Yehova, kwa ndugu na dada zetu Wakristo, na kupenda uadilifu

Mt 6:33; 1Ko 13:​4-7; 1Th 3:​12, 13; 1Yo 4:​18, 19

Kuimarisha imani yetu

Efe 6:16; 1Yo 5:4; Yud 20, 21

Kudumisha mtazamo mzuri kuelekea kuteseka

Mdo 5:​40, 41; Yak 1:​2-4; 1Pe 3:14; 4:​14, 16

Kuvumilia kwa uaminifu kuna manufaa gani?

Tunamheshimu Yehova Mungu

Met 27:11; Yoh 15:​7, 8; 1Pe 1:​6, 7

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Ayu 1:​6-12; 2:​3-5—Shetani anamshtaki Yehova kuhusu utimilifu wa Ayubu, shtaka ambalo linaweza kujibiwa tu na Ayubu anapovumilia kwa uaminifu akiwa mtumishi wa Yehova

    • Ro 5:19; 1Pe 1:​20, 21—Kwa kuvumilia kwa uaminifu hadi mwisho, Yesu anajibu swali hili muhimu: Je, mwanadamu mkamilifu anaweza kudumisha utimilifu chini ya majaribu makali zaidi?

Tunawatia moyo wengine wavumilie

Flp 1:​13, 14; Yak 5:​10, 11

Uvumilivu unatusaidia kuwa na matokeo katika huduma yetu

Mhu 11:6; Lu 8:15; 2Pe 1:​5-8

Tunapata kibali cha Yehova na baraka alizoahidi

Mt 24:13; Lu 21:19; 1Ko 15:58; Ebr 10:36

Tazama pia Ro 2:​6, 7; Yak 1:12

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki