Majina ya Cheo
Je, Wakristo wanapaswa kutumia majina ya cheo ya kidini?
Simulizi la Biblia linalohusika:
Lu 18:18, 19—Ingawa yeye ni mwema, Yesu anakataa kuitwa kwa jina la cheo “Mwalimu Mwema,” na anasema kwamba Yehova pekee ndiye mwema
Kwa nini Wakristo wanaepuka kuwaita watu kwa majina ya cheo ya kidini, kama vile, “Baba” au “Kiongozi”?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mt 23:9-12—Yesu anatukataza kutumia majina ya cheo, kama vile “Baba” au “Kiongozi”
1Ko 4:14-17—Ingawa mtume Paulo alikuwa kama baba kwa watu wengi, hakuna yeyote kati yao aliyemwita kwa jina la cheo, kama vile, Baba Paulo au majina mengine kama hayo
Kwa nini inafaa kwa Wakristo kuitana na kutendeana kama ndugu na dada?
Tazama pia Mdo 12:17; 18:18; Ro 16:1
Simulizi la Biblia linalohusika:
Mt 12:46-50—Yesu anaeleza waziwazi kwamba waabudu wenzake ni ndugu na dada zake wa kiroho
Kwa nini inafaa kwa Wakristo kutumia majina ya cheo ya viongozi wa serikali na wa kisiasa, mahakimu, na maofisa wengine wa serikali?
Simulizi la Biblia linalohusika:
Mdo 26:1, 2, 25—Mtume Paulo alipozungumza na maofisa wa serikali kama vile Agripa na Festo, aliwaita kwa majina yao ya cheo