Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • scl kur. 31-34
  • Kuhubiri Habari Njema

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuhubiri Habari Njema
  • Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
scl kur. 31-34

Kuhubiri Habari Njema

Kwa nini Wakristo wote wa kweli wanafanya tangazo la hadharani la imani yao?

Mt 28:​19, 20; Ro 10:​9, 10; Ebr 13:15

Tazama pia Mdo 1:8; 1Ko 9:16

Yesu alituwekea mfano gani katika kazi ya kuhubiri?

Lu 8:1; Yoh 18:37

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Lu 4:​42-44—Yesu anasema kwamba alitumwa duniani kuhubiri

    • Yoh 4:​31-34—Yesu anasema kwamba kazi yake ya kuhubiri habari njema ni kama chakula kwake

Je, wanaume wanaoongoza katika kutaniko ndio tu wenye jukumu la kuhubiri habari njema?

Zb 68:11; 148:​12, 13; Mdo 2:​17, 18

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 2Fa 5:​1-4, 13, 14, 17—Msichana Mwisraeli anamweleza mke wa bwana wake Msiria kumhusu Elisha, nabii wa Yehova

    • Mt 21:​15, 16—Yesu anapinga maneno ya wakuu wa makuhani na waandishi, wanaowasema vibaya wavulana wanaomsifu Yesu hekaluni

Waangalizi kutanikoni wanawezaje kuwafundisha wengine kuhubiri habari njema?

1Th 1:​5, 6; 2Ti 2:2; 1Pe 5:​2, 3

Yehova na Yesu wanatusaidiaje kutimiza kazi yetu ya kuhubiri?

2Ko 4:7; Flp 4:13; 2Ti 4:17

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mdo 16:​12, 22-24; 1Th 2:​1, 2—Ingawa mtume Paulo na waandamani wake wanatendewa vibaya, kwa msaada wa Mungu wanaendelea kuhubiri kwa ujasiri

    • 2Ko 12:​7-9—Mtume Paulo, mhubiri mwenye bidii, anasumbuliwa na “mwiba katika mwili,” huenda ni tatizo la afya; hata hivyo, Yehova anampa nguvu za kuendelea na kazi ya kuhubiri

Ni nani au ni nini kinachofanya Mkristo astahili kuhubiri?

1Ko 1:​26-28; 2Ko 3:5; 4:13

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Yoh 7:15—Watu wanastaajabu kwamba Yesu ana ujuzi mwingi ingawa hakusoma kwenye shule za marabi

    • Mdo 4:13—Mitume wa Yesu wanaonwa kuwa watu wasio na elimu na wa kawaida; hata hivyo, wanahubiri kwa bidii na ujasiri

Tunajuaje kwamba Yehova anataka tuwazoeze wengine katika kazi ya kuhubiri na kufundisha?

Mk 1:17; Lu 8:1; Efe 4:​11, 12

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Isa 50:​4, 5—Kabla ya kuwa mwanadamu, Masihi alipata mazoezi ya kibinafsi kutoka kwa Yehova Mungu

    • Mt 10:​5-7—Akiwa duniani, kwa subira Yesu anawazoeza wanafunzi wake wafanye kazi ya kuhubiri

Tunapaswa kuuonaje mgawo wetu wa kuhubiri habari njema?

Mt 11:​29, 30; 1Ti 1:12

Mkristo anahisije anaposhiriki katika kazi ya kuhubiri?

Lu 10:​1, 17; Mdo 13:​48, 52; 15:3; 20:35

Ni ujumbe gani tunaotangaza tunapohubiri?

Mt 24:14; 28:​19, 20; Mdo 26:20; Ufu 14:​6, 7

Tazama pia Isa 12:​4, 5; 61:​1, 2

Kwa nini Wakristo hufunua mafundisho ya uwongo?

2Ko 10:​4, 5

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mk 12:​18-27—Yesu anajadiliana na Masadukayo kwa kutumia Maandiko ili kuwathibitishia kwamba wana maoni yasiyo sahihi kuhusu ufufuo

    • Mdo 17:​16, 17, 29, 30—Mtume Paulo anajadiliana na Waathene ili kuwaonyesha kwamba ibada ya sanamu ni kosa

Kazi ya kuhubiri inafanywaje?

Mdo 5:42; 17:2; 20:20

Tuna msingi gani wa kuhubiri hadharani?

Yoh 18:20; Mdo 16:13; 17:17; 18:4

Tazama pia Met 1:​20, 21

Ni nini kinachoonyesha kwamba tunahitaji kuwa na subira na uvumilivu katika huduma yetu?

Isa 6:​9-11; 2Pe 3:9

Kazi yetu ya kuhubiri ina matokeo gani mazuri?

Mdo 14:​20-22; 19:​9, 10

Kwa nini inafaa kuwa tayari kutumia kila fursa tunayopata ya kuhubiri?

1Ko 9:23; 1Ti 2:4; 1Pe 3:15

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Yoh 4:​6, 7, 13, 14—Ingawa amechoka, Yesu anamhubiria habari njema mwanamke Msamaria katika kisima

    • Flp 1:​12-14—Hata alipokuwa gerezani, mtume Paulo alitumia kila fursa aliyopata kutoa ushahidi na kuwatia moyo wengine

Je, tunapaswa kutarajia kwamba kila mtu atasikiliza ujumbe wetu?

Yoh 10:​25, 26; 15:​18-20; Mdo 28:​23-28

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Yer 7:​23-26—Kupitia Yeremia, Yehova anafafanua jinsi watu Wake wanavyorudia tena na tena kutowasikiliza manabii Wake

    • Mt 13:​10-16—Yesu anafafanua kwamba kama katika siku za Isaya, wengi watasikia ujumbe lakini wataukataa

Kwa nini hatushangai kwamba watu wengi hawatusikilizi kwa sababu wana shughuli nyingi?

Mt 13:22; 24:​38, 39; Lu 17:​28, 29

Ni nini kinachoonyesha kwamba baadhi ya watu mwanzoni watasikiliza lakini hawataendelea?

Mk 4:​14-17; Yoh 6:​65, 66

Ni mifano gani inayoweza kutusaidia tusishangae baadhi ya watu wanapopinga moja kwa moja kazi yetu ya kuhubiri?

Mdo 13:50; 18:​5, 6; 1Pe 4:​12-14

Tunaitikiaje tunapokabili upinzani katika kazi yetu ya kuhubiri?

Mt 5:​10-12; 10:​14, 23; Flp 1:7

Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba baadhi ya watu watakubali habari njema?

Lu 8:15; Yoh 4:​40, 41; Mdo 16:​14, 15; 17:​11, 33, 34

Wahubiri wa habari njema wana wajibu gani mzito mbele za Mungu?

Mdo 20:​26, 27; 1Ko 9:​16, 17; 1Ti 4:16

Tazama pia Eze 33:8

Kwa nini tunapaswa kuwahubiria watu wote haidhuru dini, rangi, au taifa lao?

Mt 24:14; Mdo 10:​34, 35; Ufu 14:6

Tazama pia Zb 49:​1, 2

Je, inafaa kuhubiri siku yoyote katika juma, kutia ndani siku ya Sabato?

Mdo 5:42; 13:​42, 44; 16:13

Ni mifano gani inayoonyesha kwamba inafaa kuwahubiria watu wote, hata ikiwa wana Biblia na ni washiriki wa dini fulani?

Mdo 13:46; Gal 2:​7, 8

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki