Uadilifu
Ni nani pekee ana mamlaka ya kuamua jambo lililo sawa au la haki?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mwa 18:23-33—Yehova anamwonyesha Abrahamu kwamba Yeye ni Mwamuzi mwadilifu
Zb 72:1-4, 12-14—Zaburi hii iliyoongozwa na roho inamsifu Mfalme wa Kimasihi, ambaye anaiga kikamilifu uadilifu wa Yehova
Tunanufaikaje kwa kuishi kulingana na viwango vya Yehova vya uadilifu?
Zb 37:25, 29; Yak 5:16; 1Pe 3:12
Tazama pia Zb 35:24; Isa 26:9; Ro 1:17
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Ayu 37:22-24—Elihu anausifu uadilifu wa Yehova, ambaye ukuu wake unafanya watu wake wamheshimu sana
Zb 89:13-17—Mtunga zaburi anamsifu Yehova kwa sababu sikuzote anatawala kwa uadilifu
Inamaanisha nini kutafuta uadilifu wa Mungu?
Eze 18:25-31; Mt 6:33; Ro 12:1, 2; Efe 4:23, 24
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mwa 6:9, 22; 7:1—Noa anathibitika kuwa mwadilifu kwa kufanya kwa uangalifu mambo yote ambayo Yehova anamwagiza afanye
Ro 4:1-3, 9—Yehova anamwona Abrahamu kuwa mwadilifu kwa sababu anaonyesha imani ya pekee katika Yehova
Kwa nini ni lazima uadilifu wetu utegemee upendo wetu kwa Yehova badala ya tamaa ya kujionyesha kuwa waadilifu machoni pa wanadamu?
Mt 6:1; 23:27, 28; Lu 16:14, 15; Ro 10:10
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mt 5:20; 15:7-9—Yesu anawaambia watu wawe waadilifu, lakini si kwa kutegemea viwango vilivyowekwa na waandishi na Mafarisayo ambao ni wanafiki
Lu 18:9-14—Yesu anatoa mfano ili kuwarekebisha wale wanaojiona kuwa waadilifu zaidi na kuwadharau wengine
Kwa nini sifa ya wema ni bora zaidi kuliko sifa ya uadilifu?
Tazama pia Lu 6:33-36; Mdo 14:16, 17; Ro 12:20, 21; 1Th 5:15