Kusuluhisha Hali ya Kutoelewana
Mtu anapotukosea, kwa nini tunapaswa kuepuka kukasirika au kulipiza kisasi?
Met 20:22; 24:29; Ro 12:17, 18; Yak 1:19, 20; 1Pe 3:8, 9
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
1Sa 25:9-13, 23-35—Nabali anapomtukana Daudi na wanaume wake na kukataa kuwasaidia, Daudi anafanya maamuzi ya haraka-haraka ya kutaka kumuua Nabali na wanaume katika nyumba yake, lakini ushauri wenye hekima wa Abigaili unamsaidia Daudi kuepuka hatia ya damu
Met 24:17-20—Akiongozwa na roho, Mfalme Sulemani anawaonya watu wa Mungu kwamba kushangilia maadui wetu wanapoteseka ni jambo lisilomfurahisha Yehova; tunaacha kazi ya kuhukumu mikononi mwa Yehova
Ikiwa Mkristo amekosana na mtu, je, anapaswa kuepuka kuzungumza naye au kumwekea kinyongo?
Law 19:17, 18; 1Ko 13:4, 5; Efe 4:26
Simulizi la Biblia linalohusika:
Mt 5:23, 24—Yesu anaeleza kwamba tunapaswa kujitahidi sana kufanya amani pamoja na ndugu ambaye ana jambo fulani dhidi yetu