Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 12/15 kur. 572-573
  • “Upendo Hujenga”—Nani na Na Namna Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Upendo Hujenga”—Nani na Na Namna Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Habari Zinazolingana
  • Upendo Ni Sifa Yenye Thamani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Endeleeni Kuonyeshana Upendo​—Unajenga
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Mjengwe na Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • “Endeleeni Kutembea Katika Upendo”
    Mkaribie Yehova
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 12/15 kur. 572-573

“Upendo Hujenga”​—Nani na Na Namna Gani?

LO! NAMNA yalivyo na maana, namna yalivyo kweli maneno hayo mawili: “Upendo hujenga”! Upendo unajenga akili na mwili; vile vile unajenga kwa adili na kiroho. Mara kwa mara maneno hayo ya mtume Paulo yametumiwa kwa matokeo ya moyoni ambayo upendo unakuwa nayo juu ya walio wagonjwa wa akili na wa kimwili, na si bila sababu nzuri.​—1 Kor. 8:1.

Mfano wa ushuhuda mwingi juu ya uwezo wa upendo wa kujenga ni maneno ya Daktari Leo Bartemeir. Kama msimamizi wa chama cha wagonjwa wa akili, wakati mmoja alitaja kwamba upendo wapaswa uwemo kati ya dawa za tabibu pamoja na zile za kuua vidudu na za kuchanjia. “Upendo wa tabibu kwa mgonjwa wake na upendo wa mgonjwa kwa tabibu wake ni maongozi yenye nguvu katika kuponywa kwa wagonjwa,” akasema. Yeye anashikilia kauli ya kwamba maelekeo ya kisasa ya matabibu kuwa wenye chuki au wenye kujitenga wanaposhughulika na wagonjwa wao ni kosa na kwamba “upendo wa tabibu kwa wagonjwa wake ndiyo njia iliyo kuu na ya muhimu ya kuwaponya.”

Lakini, ijapokuwa ni kweli kwamba kwa upendo twaweza kujenga wengine, haielekei hivyo mtume Paulo alivyokuwa akiandika. Katika mstari ule ule anasema kwamba “ujuzi huleta majivuno.” Kwa kuwa Paulo alimaanisha kwamba namna fulani ya ujuzi ilielekea kuwatia majivuno wale waliokuwa na ujuzi huo, bila shaka alimaanisha katika habari inayozungumzwa sasa kwamba upendo unajenga wale walio nao; kwamba wale ambao wangeonyesha upendo wenyewe wangefaidika kwa njia hiyo. Kwa kweli, katika mtajo uliotangulia wa Daktari Bartemeir uhakika huu waonekana. Namna gani hivyo? Kwa sababu anasema si kwamba tu upendo wa tabibu unamjenga mgonjwa bali pia upendo wa mgonjwa unamjenga yeye mwenyewe, si tabibu! Katika maana ii hii mchunguzi wa desturi a watu Ashley Montagu aliandika kwamba “upendo ni wenye kujenga, ukitajirisha sana maisha za mpokeaji na mpaji vile vile.”

Kinachoushuhudia zaidi ukweli wa maneno ya Paulo kwamba “upendo hujenga” ni kitabu cha dawa ya moyo cha Wataalamu Weiss na English: “Mtu aliye na uwezo wa kupenda kwa kawaida naye anapendwa. Uwezo wa kuonyesha nia njema na kufikiria wengine katika kila upande wa maisha, ya kijamaa, ya ndoa, yapasayo mume na mke na ya uzazi, una matokeo yenye kumjenga sana mtu anayeuonyesha upendo huo na vile vile mtu anayeupokea na kwa njia hiyo wawaletea wote wawili furaha.” (Maneno yaliyo na chapa tofauti yameandikwa vile kuonyesha maana.) Ndiyo, kama vile wachimbuzi wa mambo ya kale (archaeologists) wanavyozidi kufanya mavumbuzi yanayohakikisha maandishi ya kihistoria ya Biblia, ndivyo na matabibu wa akili wanavyouhakikisha usawa na hekima ya shauri la Biblia juu ya ujamaa wa kibinadamu.

Kuwaza kidogo kutaonyesha wazi namna ilivyo kweli kwamba upendo unamjenga yeye anayependa. Muumba wetu mkuu na mwenye upendo na hekima alitia ndani yetu utaratibu wa chembe zilizomo damuni zinazofanya kazi vizuri zaidi tunapoishi kulingana na kanuni zake za haki na za hekima. Sayansi ya watu wenye magumu ya akili imeonyesha dhara linalomjia mtu anayejitia katika mambo kama vile ukorofi, hasira, uchungu, pupa, kujisikitikia, kijicho na kukata tamaa. Yajapokuwa yawadhuru wengine, yanamdhuru zaidi yeye anayeshindwa na mambo hayo.

Kwa busara basi, lazima iwe kwamba tunapoonyesha maono ya ndani yafaayo na yenye kujenga, ambayo yaliyo makuu ni upendo usio wa kichoyo, twajenga si wengine tu bali zaidi sisi wenyewe, kama inavyoonyeshwa katika maneno ya Bwana Yesu: “Ni heri kutoa kuliko kupokea.”​—Matendo 20:35.

Ijapokuwa ni kweli kwamba upendo kwa mwenzi wako, kwa jamaa yako na kwa rafiki mkubwa waweza kukujenga wewe, kutokana na matumizi ya mtume ya neno la Kigiriki agápe ni wazi kwamba alikuwa akiumaanisha upendo usio wa kichoyo na unaoongozwa na kanuni, usiofikiria mambo ya mtu peke yake. Kwamba upendo huu unajenga yazidi kuonekana kwa anavyousimulia. Anasimulia kwamba namna hii ya upendo ni ya uvumilivu, ni yenye subira na yenye fadhili, kwamba yaweza kuvumilia yote na kwamba haishindwi. Unaosaidia kuonyesha zaidi upendo unajenga ni uhakika wa kwamba unaondoa maono ya ndani yenye kulegeza kama vile majivuno, wivu na pupa.​—1 Kor. 13:4-8.

Upendo usio wa kichoyo kwa Yehova Mungu na kwa jirani yetu utatuwezesha kuzuia vishawishi vya kufanya mabaya au kufuata mwendo wa kujitumikia wenyewe, ambao huenda ukawa ni “halali” kabisa lakini usiotujenga. Tunapozitegemeza kanuni zetu, mawazo yetu makamilifu, tunapopata ushindi juu ya maelekeo yetu ya kichoyo na ya kutokamilika, si kwamba tu twashika dhamiri safi lakini vile vile twajengwa kwa njia ya adili na kiroho. Ndipo tunapoweza kuiona mithali iliyoongozwa na roho ya Mungu kuwa kweli kwa habari yetu: “Wenye haki ni wajasiri kama simba.” Kama vile Ayubu wa kale tutaweza kuwakanusha wale wanaoshindana na makusudi yetu, nasi tutaweza kukiri kuwa na dhamiri njema mbele za Mungu.​—Mit. 28:1; Ayubu 16:1-4; 29:l-25.

Huenda vile vile upendo ukasemwa unajenga kwa maana unakuwa mwepesi kumthawabisha mtu aliye nao. Si kwamba hiyo ndiyo sababu ya kuonyesha upendo, bali yaelekea sana kwamba hayo ndiyo yatakayokuwa matokeo. Kama vile Yesu Kristo alivyosema: “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; . . . Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.” (Luka 6:38) Mwanamke ajulikanaye sana ambaye ni mtaalamu wa magumu ya akili aliandika kitabu cha kushauri wanawake wenye huzuni walioolewa, nacho kilionyesha kwamba kupenda waume zao kwa njia ya kweli na kuwanyenyekea ndilo jambo lenye kuthawabisha zaidi ambalo wangeweza kufanya. Washiriki wa jamaa wanaweza kupata furaha kwa kujitahidi waleteane furaha mmoja na mwenzake.

Huu ni mfano mwingine wa Maandiko wa kanuni hii ya Biblia. Alipokuwa akiwatia moyo Wakristo wenye utajiri wa kimwili katika Korintho waonyeshe upendo usio wa kichoyo kwa ndugu maskini katika Yerusalemu, mtume Paulo aliandika hivi: “Yeye apandaye . . . kwa wingi atavuna kwa wingi pia.”​—2 Kor. 9:6.

“Upendo hujenga”​—nani? Bila shaka unajenga mpokeaji mwenye shukrani, lakini unajenga mpaji hata zaidi, yeye apendaye. Mpaji anajengeka kwa kila njia, kimwili, akilini, moyoni na kiroho. Anavuna kwa wingi naye anapendwa na Mungu, kwa maana “Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.”​—2 Kor. 9:7.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki