Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 7/15 kur. 327-328
  • Je! Wewe Unaihurumia Jamaa Yako Kama Unavyowahurumia Wengine?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unaihurumia Jamaa Yako Kama Unavyowahurumia Wengine?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Habari Zinazolingana
  • Kufanikisha Maisha ya Jamaa
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Mume Anayejipatia Heshima Nyingi
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Jinsi ya Kufanya Maisha ya Familia Yako Yawe Yenye Furaha
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Mpango wa Yehova wa Familia Wenye Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 7/15 kur. 327-328

Je! Wewe Unaihurumia Jamaa Yako Kama Unavyowahurumia Wengine?

“NAFURAHI kwa vile umeweza kufika,” kasema mwenye nyumba mkaribishaji kwa mmoja wa wageni wake. Mgeni kaitikia hivi: “Mimi nikisema n’takuja, NINAKUJA!” Ndiyo, alijivunia kuwa mtu mwenye kutimiza ahadi yake. Lakini je! alikuwa mtu mwenye kutimiza ahadi kwa jamaa yake? Si sikuzote.

Kuna mithali ya Kijeremani inayosema, Haus Bengel und Strassen Engel, maana yake, ‘Nyumbani ni mshenzi lakini njiani ni malaika’ au mwungwana. Mithali hiyo inaonyesha makosa ya wanadamu wote. Kwa mfano, huenda mwishoni mwa jioni ya starehe mume akapenda kumsaidia kijana mwanamke asiyeolewa kuvaa koti lake, lakini akamwacha mkewe ajivike koti lake mwenyewe. Inaonekana kama yule mwanamke mrembo asiyeolewa alimpendeza sana mume huyo hata akawa mwungwana. Heri angeweza kuwa mwenye huruma na mwungwana kwa mke wake! Huko kungekuwa ndiko kumpenda mke wake kama anavyojipenda mwenyewe, jambo linalompasa mume kufanya.​—Efe. 5:33.

Pamoja na jambo hilo ni usemi wa kwamba “wema unaanzia nyumbani,” yaani, umepaswa uanzie nyumbani. Si lazima kutoa fedha, bali kuwa wenye kusaidiana. Je! hatuwi wepesi kusaidia wakati mgeni anapouliza njia au habari fulani nyingine? Je! haitupasi vile vile tuwe wepesi kusaidia katika nyumba zetu, hata kuwa tayari zaidi kufanya hivyo? Lakini ni mara nyingi mshiriki mmoja wa jamaa ndiye anayeshughulika na kazi na huku wengine wa jamaa hawaoni nafasi zao ili wasaidie. Je! wako watoto fulani wanaotaka kutayarishwa mbele ya wakati fulani? Je! kuna sahani nyingi zinazotakiwa kusafishwa? Zaidi imewapasa waume wenye “wake wanaofanya kazi” wafahamu kwamba ni lazima waondoe yale mawazo ya kwamba hii ni kazi ya wanaume na hii ni kazi ya wanawake, ikiwa wake hawatalemewa isivyofaa.

Wema vile vile unaanzia nyumbani wakati wa kuvumilia udhaifu na makosa ya wengine. Pengine mtu ataelekea kuwavumilia rafiki zake walio nje na wale anaojuana nao, kama wale anaofanya kazi pamoja nao. Je! si afadhali tuwe tayari na wenye nia hata zaidi kuvumilia makosa na udhaifu wa jamaa zetu wenyewe? Mara nyingine huenda ikawa ni kutofahamu sawasawa wajibu na upendo ndiko kunakowafanya wake au waume wengine kuwa wenye kuwalaumu wenzi wao isivyofaa.

Ni jambo la maana zaidi sana kujengana kwa kusaidiana, kusahau makosa madogo madogo, kuliko kwamba ni lazima kila jambo liwe kamili kabisa au lilingane kabisa na tunavyofikiri lapaswa liwe. Zaidi, mwenye kuelekea kumtoa mwingine makosa huenda akawa ndiye mwenye makosa. Ndiyo, mtu aliye karibu na mwingine aweza kuwa mwenye msaada katika kumsaidia yule aepuke makosa, lakini kumlaumu mwenzi wako kwaweza kuwa kubaya. Ndiyo, jambo la kufikiria kufanya ni kuvumilia makosa ya wengine. Kumbuka, mara nyingi yanatokea kwa sababu ya kurithi au kwa sababu ya mazingira, yanayofanya mikazo katika kumgeuza mtu. Na huo vile vile ni mwendo wenye hekima, kwa maana kwa kadiri tutakavyokuwa wenye kuwarehemu wengine, ndivyo wengine watakavyoturehemu sisi, hata kama Yesu Kristo alivyosema pindi moja: “Kipimo kile kile [mwapimiacho wengine] ndicho mtakachopimiwa.” (Luka 6:38) Kama mwanamke mmoja wa Kiamerika katika gazeti alivyosema katika kupinga maoni ya wengine katika chama cha ukombozi wa wanawake: “Mimi namtendea mume wangu kama mfalme naye anitendea kama malkia.”

Usemi wa ulimwengu wa kwamba “utani huleta dharau” au kuzoeana sana kunaleta dharau, usitumiwe katika uhusiano (ukamatano) wetu na washiriki wa jamaa yetu. Utani au kuzoeana sana kumepaswa kulete uaminifu na heshima kwa sababu tumejifunza kujuana na kufahamiana vizuri zaidi. Ni kawaida kwa watu ambao wamepewa malezi yanayofaa nyumbani wakati wa utoto kuwatendea watu wa nje kwa heshima. Na hivyo ndivyo ipasavyo kuwa, kwa maana je! Biblia haisemi, “Waheshimuni watu wote”? “Watu wote” wangetia washiriki wa jamaa zetu wenyewe, sivyo? (1 Pet. 2:17) Kwa kuonyeshana heshima, washiriki wa jamaa wanatiana nguvu wao kwa wao, wakimwezesha kila mmoja awe mwenye kusaidia wengine. Heshima yaweza kuonyeshwa kwa kuwataja wengine kwa heshima inayolingana na walivyo na maoni yao, katika yanayosemwa na namna yanavyosemwa.

Mara nyingine mshiriki wa jamaa anajiona huru kuropoka, kuwa mkali au mwenye kulaumu wengine katika jamaa ingawa asingefikiria kuwatendea watu wa nje kwa njia hiyo. Lakini, katika kufanya hivyo, je! haonyeshi kuwa anakosa huruma? Kwa mfano, kuna tofauti kubwa kati ya namna tunavyoona wakati tunapojikuta tumefanya kosa, na twaweza kuliondoa, na namna tunavyoona wakati mwingine anapotuonyesha kosa na atuomba tuliondoe. Huruma itatusaidia tufahamu tofauti hiyo.

Walakini, mara nyingi kushindwa kwetu kuwatendea jamaa zetu kama tuwatendeavyo watu wa nje ni kwa sababu ya kutofikiri. Zaidi wakati wa kusema mambo ambayo heri yasingalisemwa. Kwa watu wa nje tunaelekea kuwa waangalifu zaidi. Lakini kwa jamaa zetu wenyewe inafaa vile vile kufikiri sikuzote mbele ya kusema. Kanuni iliyo karibu ni kujiuliza: “Je! ni fadhili? Je! ni kweli? Je! ni lazima?” Fikiria, vile vile, unavyolisema jambo. Kinyume cha kutofikiria ni kuonyesha kufikiria au huruma. Fanya hivyo hata katika mambo madogo, kwa maana mambo madogo yanamaanisha mengi. Huruma inaonyeshwa kwa kutangulia kuomba “Tafadhali,” na kusema “Asante!” na kuwa ndivyo unavyomaanisha wakati wo wote unapopokea fadhili bila kujali ziwe ndogo.

Ni nyingi sana sababu za kutufanya tuwe wenye msaada, wenye kuonyesha wema, wenye kuheshimu na kuhurumia katika kushughulika na wale walio nje ya jamaa zetu. Kuna uradhi katika kuonyesha sifa hizi, unafanya hali ziwe bora, unatusaidia tufikiriwe na hata unaweza kutufaidi katika njia ya kimwili. Lakini je! hatufaidiki vile vile katika njia hizi mbalimbali ikiwa twawaonyesha wale wa jamaa zetu sifa hizi? Ndiyo, na hata zaidi sana. Zaidi ya hayo, katika kufanya hivyo twaweza kusemekana kuwa ‘tukiweka hazina’ ambazo zaweza kuchukuliwa wakati tunapokuwa katika shida. Na hiyo yaweza kuwa faraja kama nini!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki